Barcelona Kuvunja Dili la Mkopo January!

Barcelona wanatajwa kuwa kwenye mpango wa kumalizana na nyota wao wa mkopo Yusuf Demir kabla ya dirisha la usajili la Januari.

Demir alijiunga na Barca kwa mkataba wa mkopo wa msimu mzima kutoka Rapid Wien msimu wa joto, na dili hilo pia lilihusisha chaguo la kumnunua kwa euro milioni 10.

Tangu wakati huo, kinda huyo mwenye umri wa miaka 18 amecheza mechi sita pekee za La Liga akiwa Barcelona, licha ya kwa wababe hao wa Catalan kutofanya uamuzi wa kumnunua chaguo, wamepanga kumaliza muda wake wa mkopo mapema zaidi.

Yusuf Demir

Kwa mujibu wa Sport, Barcelona tayari wamemwambia Demir kwamba anakaribishwa kutafuta klabu mpya, na inaonekana atabadilisha vilabu kwa mkopo katika dirisha la Januari.

Kulingana na ripoti hiyo, Borussia Dortmund, Eintracht Frankfurt na Bayer Leverkusen wote wanatajwa kuwanawania saini ya winga huyo.

Barcelona wanajaribu kuweka sawa vitabu vyao vya fedha kabla ya dirisha la Januari na kumalizana na Demir, licha ya kutolipwa pesa nyingi, unakuwa mwanzo mzuri kwao.


ANZA MSIMU WA SIKUKUU NA BURST THE BANK

Fanya wiki yako iwe ya ushindi mkubwa ndani ya kasino za mtandaoni za meridianbet. Mchezo wa BURST THE BANK🔥🤑 ni moja kati ya mchezo pendwa unaowapa wachezaji mamilioni kila siku. Kwa dau dogo unashinda zaidi.

tetesi, Tetesi za Soka Barani Ulaya., Meridianbet

CHEZA HAPA

Acha ujumbe