Christian Eriksen: Hii Siyo Ndoto Niliyoota Milan

Nyota Christian Eriksen amebainisha kuwa kinachoendelea kwake Inter Milan ‘sio kile alichokiota’ na yuko tayari kwa uhamisho wa dirisha la Januari ikiwa hatapewa mda zaidi wa kucheza.

Kiungo huyo ambaye yupo kwenye jukumu la kitaifa na Denmark, alizungumza na TV2 Sport juu ya kutokuwa na mchango mkubwa chini ya Antonio Conte.

“Hapana, hiki sio kile nilichokiota,” alikiri nyota huyo wa zamani wa Tottenham Hotspur.

“Nadhani wachezaji wote wanataka kucheza kadri inavyowezekana, lakini mwishowe kocha anaamua ni nani atakayeingia uwanjani.”

“Ni hali kubwa ya kushangaza, kwani mashabiki wanataka kuniona nikicheza zaidi na mimi pia, lakini kocha ana maoni tofauti na kama mchezaji lazima niheshimu hilo.” – Christian Eriksen

Christian Eriksen

Christian Eriksen anasema kuwa kimsingi, Inter kwa sasa mambo hayaendi, lakini pia anakubali kuwa alipokuwa nje ya timu ilikuwa inapata ushindi, lakini hii haimaanishi uwepo wake ndiyo unaikwamisha timu kwa sasa.

Lakini, hakujaribu kuficha uwezekano wa kuondoka Januari, wakati PSG wakitajwa kuwa inavutiwa na huduma yake.

“Kwa sasa, ninazingatia soka langu tu, kisha tutaona wakati dirisha la uhamisho likifunguliwa ikiwa kuna jambo litatokea au la.” – Christian Eriksen


 

UMEJARIBU HII POKER YA VIDEO?

Jaribu sasa hapa Meridianbet. Ukiacha ukweli kuwa itakupa burudani maridadi, bado inakuhakikishia ushindi mkubwa. Kazi kwako kukusanya ushindi!

Meridianbet Casino

INGIA MCHEZONI!

22 Komentara

    Sio kila unachokiota lazima kiwe vile vile so relax

    Jibu

    Inaoneka kocha hajapendekezwa na kazi yake Eriksen na ndio maana hamekua hampi number kwenye kikosi ukiangalia wachezaji wengi sana chipukizi mwenye umli mdogo tu ukiachiliana mbali na humri halio kua nao

    Jibu

    Awe mpole tu

    Jibu

    Atulie tu

    Jibu

    Kuwa na subila jembe ndoto zako Zita timia

    Jibu

    Inabidi aheshimu maamuzi ya kocha atulie tu

    Jibu

    eriksen alikuwa na matarajio makubwa sana ilaa anaona yanaenda sivyo

    Jibu

    Huwezi kuota ndoto ikatimia yote nyingine .huishia njiani kwa hiyo awe tu mpole

    Jibu

    Uko sahihi kabisa kwa upande mwingine tunawatupia lawama makocha ila kwa vingine nasema kuwa kama shirika la michezo la upande wa mpira wa mguu wangeweka idadi ya kubadili wachezaji 5 kama mwanzo ingekuwa vizuri mana wachezaji wengi wangepata nafasi lakini ni 3 tu inabidi lawama tuwape wengine kocha huwa anatimiza jukumu lake tu na wachezaji wote wanapenda kucheza mpira

    Jibu

    Eriksen alitaka changamoto mpya, nadhani hiki ndicho alichohitaji nacho ni kupigania namba

    Jibu

    Subira yavuta kher

    Jibu

    Erikson alifany makosa makubwa sana kuondoka spurs ilibid ajaribu kuangaliah upepo jinsi ulivyo sasa noana mambo yanazid kwenda kombo ndani ya milan naiman czan Kama January ataendeleah kusaliah milan

    Jibu

    Erikson anandoto ya kufika mbali sasa kocha wake anamuweka benchi sana

    Jibu

    Awe mpole tu

    Jibu

    Eriksen anajua kazi yake intet. Imepata mtu

    Jibu

    Inabidi awe mpole kwanza

    Jibu

    Avute subira

    Jibu

    Erikson alifanya makosa makubwa kuondoka totenham

    Jibu

    Goodupdate

    Jibu

    Itabidi tu awe mpole

    Jibu

    Inter imepata kiingo fundi na amekua kwenye kiwango bora toka msimu wa mwisho alivyokiwa totenham

    Jibu

    Atutulie

    Jibu

Acha ujumbe