Klabu ya manchester United imetambilisha rasmi namba ya jersey ya kiungo wa mpya alisajiriwa kwa uhamisho huru baada ya kumaliza mkataba wake na klabu ya Brentford Christian Eriksen na kupewa jersey namba 14.
Manchester wametangaza jersey mpya Eriksen baada ya kutangaza jersey namba ya mlinzi mpya wa klabu hiyo aliyesajiriwa akitokea ajax Lisandro Martinez ambaye anatarajiwa kuvaa namba 6.
Awali ilisemekana kuwa Christian Eriksen angepewa Jersey namba 8, baada ya kuondoka Juan Mata yeye angekabidhiwa jersey hiyo, badala yake jersey hiyo imechukuliwa na Bruno Fernandes.
Mpaka sasa jersey namba 14 imevaliwa na wachezaji 41 wakiwemo makipa wawili ambao ni Tim Howard na Andy Goram huku majina makubwa ambao walishai kuvaa jersey namba 14 ni Nicky Butt, Alan Smith, David Beckham, Mark Hughes, Chicharito, Jesse Lingard, Gary Neville, Jordi Cruyff, Paul Scholes, Mike Phelan na Ryan Giggs.