Matthijs de Ligt anasema anajaribu kujifunza kutoka kwa wanatimu wenzake wa Juventus, Leonardo Bonucci na Giorgio Chiellini.
Kinda huyu mwenye miaka 20 ameweka wazi kuwa mwanzoni halikuwa lengo lake kucheza kama mlinzi. De Ligt alifika Juventus msimu wa joto uliopita akitokea Ajax kwa paundi milioni 85.
Tangia kufika klabuni hapo anasema anajifunza mambo mengi zaidi na kuendelea kujiboresha. Amebainisha kuwa katika vitu vingine vingi, kujitambua kwake imekuwa nguzo ya mafanikio, na anaamini hii itampigisha hatua ndefu zaidi.
“Ni vyema kujitamba mwenyewe kama akili yako iko sawa. Kama uko tayari, hakuna anayeweza kukuzuia” Aliliambia jarida la Champions Journal.
Kama mlinzi makini, alihitaji kujua ni mambo gani mazuri ayafanye, na kurejea nyuma kujifunza kupitia makosa, na hufanya hivyo mara nyingi.
Licha ya kuwa na umri mdogo tayari kinda huyu ameshacheza na mastaa wengi wakubwa, kwa nafasi yake wakiwepo akina Virgil van Dijk kwa Netherlands, pamoja na Bonucci na Chiellini hapo Juventus.
Hadi alipokuwa na umri wa miaka 15, De Ligt alikuwa anacheza kama kiungo mshambuliaji hadi aliposhauriwa kubadilisha nafasi hiyo.
“Nilicheza sana kama kiungo, nilifunga magoli, nilitoa asisti, na ghafla wakaniambia kuwa ingekuwa vyema kwa kazi yangu ningeenda nafasi ya ulinzi, katikati.”
Wenyewe wanasema mipango siyo matumizi! Staa huyu anafurahia nafasi yake kwa sasa kama mlinzi na anaendelea kujifunza mengi licha ya ukweli kwamba hakuwahi kuwaza hivyo awali.


Antony luseno
ktk soka mwalimu ndo uwa anaweza kuona mbali uenda ktk safu ya ulinzi utafanya vyema zaidi
Ernest Kimeru
Matthijs de Ligt Jicho lengine kwenye ulimwengu wa Soka!!!!
Furahav
Beki kisiki huyo