Bayern Munich Kuingia Sokoni Januari

Mkurugenzi wa klabu ya Bayern Munich amethibitisha kua klabu hiyo itaingia sokoni katika dirisha dogo la usajili mwezi Januari ambapo wataboresha maeneo kadhaa katika kikosi chao.

Mkurugenzi Freund amesema timu hiyo inahitaji maboresho katika maeneo kadhaa hivo mwezi Januari lazima waingie sokoni kwajili ya kuboresha kikosi chao na kupambania mataji msimu huu.bayern munichBayern Munich ina mpango wa kuingia sokoni mwezi Januari na vipaumbele vya ni kiungo wa Ulinzi na beki wa katikati, Hii ni kutokana na taarifa ya mkurugenzi wa klabu hiyo bwana Freund ambaye ni mtendaji mpya klabuni hapo.

Klabu hiyo ambayo ipo chini ya kocha Thomas Tuchel toka mwezi Machi mwaka huu imekua haina mwenendo mzuri sana, Huku kiungo Joshua Kimmich akiwa hana mbadala wa uhakika klabuni hapo ndio sababu ya kuhitaji kumtafutia mtu wa kusaidiana nae majukumu.bayern munichAidha klabu ya Bayern Munich itaangazia beki wa katikati kwani klabu hiyo imekua ikruhusu mabao sana siku za karibuni, Hivo pia watahitaji kusajili beki mwingine wa katikati kwajili ya kuhakikisha wanatengeneza ukuta mgumu klabuni hapo.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.