Robert Lewandowski ameweka rekodi mpya kwenye ligi kuu ya Ujerumani Bundesliga kwa msimu mmoja wa 2020/21 baada ya kufunga magoli 41 kwa msimu na kuipita rekodi ya mkongwe Gerd Müller ambaye alifunga magoli 40 kwa msimu.
Gerd Müller aliweka rekodi ya kufunga magoli 40 kwenye msimu wa 1971/72, ambapo alizua mbishano mengi yaliyotokea kwamba isingewezekana kufikia kwa mchezaji mwingine kufikisha, baadae ya Dieter Müller alimkaribia kwenye msimu wa 1976/77 akiwa na msimu mzuri na klabu ya Cologne akifunga magoli 34 kwa msimu.

Robert Lewandowski msimu wa 2019/20 aliweza kuifikia rekodi ya Dieter Müller, baada ya kufunga magoli 34 kwenye michezo yote aliyoichezea klabu ya Bayern Munich huku akiwa amekosa michezo mitatu tu kwa msimu huo.
Sasa ni Robert Lewandowski ambaye anashikilia rekodi ya kufunga magoli mengi ndani ya ligi ya BUndesliga, baada ya kupindua rekodi ya Gerd Müller ambayo ilikaa takribani miaka 50, je ataweza kuipiku rekodi yake mwenyewe kwa misimu ijayo kwa umri alinao wa zaidi ya miaka 30?
Nani hapendi kuwa bingwa na kujishindia mkwanja wa kusahato kuelekea katika sikukuu wiki hii. Mchezo wa Ocean Call kutoka kasino maridhawa za meridianbettz unakupa kila sababu ya kuifanya siku kuu yako kuwa ya kuvutia zaidi.


