Klabu ya Barcelona imepewa barua ya onyo na kutoka kwenye chama kinachosimamia haki za wachezaji nchini Hispania “AFE Spanish Players Union” baada ya ya kumpa presha Ousmane Dembele kama hataki kusaini aomdoke baada ya kushindwa kukubaliana mkataba mpya.
Onyo limetokana na kauli ya mkurugenzi wa michezo Mateu Alemany siku ya alhamisi alinukuliwa akisema, “tumemwambia kuwa ni lazima aondoke klabuni haraka iwezekanavyo” baada ya kushindwa kukubaliana mkataba mpya.

Kocha wa timu ya Barcelona Xavi Hernandez anahisi kuwa alidanganywa na mchezaji huyo na kumpa barua ya onyo ya mwisho siku ya jumatano, huku ikioneka mwisho wa mfaransa huyo kwenye viunga vya Camp Nuo hauna tamati nzuri.
Waraka waliotoa “AFE Spanish Players Union” ulisomeka, kutokana na, mahusiano waliyonayo na kati ya FC Barcelona na mchezaji Ousmane Dembele shirikisho linataka kuelezea yafuatayo.
AFE kulingana na sheria za usajiri wa mkataba wa mchezaji wa kimataifa, mchezaji anawajibika kutoa huduma kwa niaba ya klabu yake maeleze yanatolewa kama ifuatavyo, klabu inapaswa kkumlipa mshahara wake kama walivyokubaliana chini ya masharti yale yale waliyokubaliana.
Hakutakuwa na ubaguzi wowote au kumlazimisha, mchezaji kuvunja sheria za kazi, tunaelewa kwamba kunahitajika kusaini mkataba mpya kwa pande zote mbili, makubaliano inabidi yawe huru kwa pande zote mbili kukubaliana na pasiwepo nguvu yeyote kutoka nje inayotoa masharti ya ukomo wa kulazimisha.
Ni muda wako kujiachia na mchezo maridhawa wa Almighty Aztec katika kasino bomba za meridianbettz. Nafasi ya kutengeneza mkwanja iko mikononi mwako kazi ni kwako.

CHEZA HAPA

