Mlinzi wa Atletico Madrid na Uingereza, Kieran Trippier amefungiwa kwa wiki 10 kujishughulisha na soka na anatakiwa kulipa faini ya £70,000 kwa kukiuka sheria za Shirikisho la Soka (FA) juu ya masuala ya Ubashiri.
Tamko la FA limethibitisha juu ya uamuzi huo wa kumsimamisha kwa wiki 10.
Nyota huyu mwenye miaka 30 hatatakiwa kushiriki kwenye shughuli zozote za kimichezo mara tuu baada ya hukumu hiyo kutoka, na athabu yake itadumu hadi Februari 28, 2021.
Kieran Trippier alikuwa anatuhumiwa kwa makosa 7 yanayohusiana na kukiuka vipengele vya masharti ya sheria za FA (FA Rule E8 [1][b]) mwezi Julai 2019. Katika makosa hayo aliweza kukana makosa yote lakini makosa manne yalipatikana kuwa na ushahidi na kupelekea maamuzi ya adhabu hiyo.
Kutokana na adhabu hiyo, staa huyu atajikuta anakosa takribani mechi 14 za La Liga, na mechi moja ya mzunguko wa Ligi ya Mabingwa hatua ya mtoano wa timu 16 dhidi ya Chelsea.
Kwa maana hii, Trippier anatarajia kurejea tena dimbani wakati Atletico wakiwakaribisha Real Madrid kwenye El Derbi Machi 7.
VUNA SHEA YAKO YA 230,000,000TSH NA UFURAHIE MSIMU HUU WA SIKUKUU!!!
Kupitia Kasino ya Mtandaoni ya Meridianbet, jiwekee nafasi ya kupata shea yako ya 230,000,000Tsh kupitia mchezo wa Secret Santa. Hakika hutojutia kufurahia msimu huu wa sikukuu ukiwa katika nyumba ya mabingwa ya Meridiabet. Unasubiri nini???
Lydia Emmanuel Magoti
Duu sio poa
Adelta
Ni vizuri kwa wengine ili wajifunze
warda
pole yake jamani
Shakila mrope
Mhh anatia huruma
Rahmal
Aise majanga kweli pole yake
Ernest Kimeru
Kieran Trippier mtukutu sana
Saupha mohamed
Jamaa mtukutuka sana
Issa
Pengo kwa jose
Hopemwaikuka
So sad
Tatu
Pole yake
Sarah
Mh pole yake