La Liga Kupambana Dhidi ya Man City na PSG

Shirikisho la soka nchini Hispania limeingia kwenye vita na vilabu vya Paris Saint Germain ya nchini Ufaransa na Manchester City ya nchini Uingereza kwa kwenda kuishitaki kwenye shirikikisho la soka nchini Ulaya kwa vilabu hicyo kuvunja sheria ya  ‘Financial Fair Play’.

Raisi wa La Liga Javier Tebas alianza kuilalamikia klabu ya PSG baada ya klabu hiyo kuweza kumshawishi mchezaji nyota Kylan Mbappe kubaki kwenye timu hiyo ambapo awali mchezaji huyo alikuwa anahitajika na klabu ya Real Madrid.

Baada ya kumkosa na mshumbuliaji kutoka timu ya Borrusia Dortmund, ndipo moto ulipowaka haikuwa tena vita ya vilabu ambavyo vimewakosa hao wachezaji, imekuwa kati ya shirikisho la soka nchini hispania La Liga dhidi ya PSG na Man City sasa.

Sababu kubwa ambayo imewapelekea La Liga kupeleka kesi UEFA ni ‘Financial Fair Play’ ambapo sio kweli hiyo sababu imetumika kama mwamvuli wa kujitetea kwa vilabu vyake vikubwa kushindwa kushawishi majina makubwa kujiunga na vilabu hivyo.

La Liga wanaona kuwa vilabu vyake vikubwa ambavyo ni Barcelona na Real Madrid kukosa majina yenye mvuto kwenye soka, kutapunguza mvuto na ufwatiliaji wa soka la nchini humo na kupunguza mikataba ya kibiashara.

Kuondoka kwa wachezaji wenye majina makubwa nchini Hispania, pia kutofanya vizuri kwa Barcelona ambayo ina matatizo ya kiuchumi, kunapunguza mvuto wa ligi hiyo. Sasa shirikisho linajitahidi kuvuisaidia vilabu vyake kufanikisha sajiri muhimu ili kurudisha mvuto wa ligi hiyo ambao unakwenda kupotea.


ALIYA’S WISHES

Bila shaka unatamani ushindi mkubwa, vipi kuhusu kujaribu Sloti hii ya Aliya’s Wishes? jaribu ushinde sasa.Kasino ya Mtandaoni

CHEZA SASA

Acha ujumbe