Hakika usiku wa jana ulikuwa na maajabu sana hususan mashabiki wa Yanga ambao walikuwa na siku ya majonzi kabla ya kugeuzwa na kuwa siku ya furaha. Timu hiyo ilikuwa wakicheza dhidi ya Mwadui na mpaka dakika 90, wanachi 1 – Mwadui 2.
Timu ya Yanga ilikuwa ikishambulia kila dakika lango la Mwadui lakini mpaka dakika 90 hawakufanikiwa kupata mabao ya kuongoza. Ni ‘sub‘ za Wazir Junior na Yacouba Sogne ndio zilizoleta mabadiliko.
Katika dakika nne za nyongeza, Yanga ilifanikiwa kufunga magoli mawili ndani ya dakika mbili tu na kuwaacha Mwadui wakiwa wamezubaa wasijue wafanye nini.
Ushindi huo wa Yanga unamaanisha kuwa wamefikisha alama 67 zikiwa ni tatu tu nyuma ya Vinara Simba ambao wana alama 70 wakiwa na michezo mitatu mkononi.
Simba watashuka dimbani siku ya kesho kuvaana na Mbeya City pale Estadio De Benjamin Mkapa majira ya saa moja jioni, na watalazimika kuchukua alama tatu ili kujijengea mazingira mazuri ya kubeba ubingwa wa msimu huu!


