Kocha wa timu ya taifa ya Ufaransa Didier Deschamps amemkingia kifua mshambuliaji wake wa timu hiyo Kylian Mbappe baada ya kuonekana kuelezwa kua mbinafsi jambo linaloeweza kuharibu upangaji timu wa kocha huyo.
Kocha huyo ambaye anatarajia kufanya mabadiliko kwenye kikosi chake kuelekea mchezo wa mwisho wa kundi D ambao watacheza na timu ya taifa ya Tunisia siku ya Jumatano. Imelezwa mchezaji wa timu hiyo analazimisha kucheza mchezo huo
Kocha Deschamps amekanusha taarifa za kua Mbappe anaweza kuathiri upangaji wa timu yake ambayo amepanga kufanya mabadiliko kwakua tayari wameshafuzu hatua inayofuata kutokana na ubinafsi wake.
Ufaransa wamekisha kufuzu hataua inayofuata na kufanikiwa kua timu ya kwanza kwenye michuano hiyo baada ya kushinda michezo yake ya awali dhidi ya timu ya taifa ya Australia pamoja na timu ya taifa ya Denmark katika mchezo wapili.
Kocha huyo wakati anaulizwa na waandishi wa habari kuhusiana na suala hilo amekanusha na kusema mchezaji wake sio mbinafsi na hawezi kuathiri upangaji wa timu yake kwa namna yeyote ile kama ambavyo waandishi wa habari wanatangeneza mambo.
Kocha Deschamps ambaye amefanikiwa kushinda kombe la dunia na timu hiyo kama mchezaji vilevile kama kocha na mwaka huu wanapewa nafasi ya kutetea taji lao kutokana na ubora wa kikosi walichonacho.

