Messi Kuiongoza Argentina Kutwaa Ubingwa WC 2022

Lionel Messi atatengeneza mashambulizi ya hatari pamoja na Paulo Dybala, Lautaro Martinez na Julian Alvarez baada ya kujumuishwa katika kikosi chake cha tano cha Kombe la Dunia la Argentina.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 35 huenda atashiriki Kombe lake la Dunia mara ya mwisho baada ya kucheza michuano yake ya kwanza mwaka 2006, na bado hajashinda HATA moja.

 

Messi Kuiongoza Argentina Kutwaa Ubingwa WC 2022

Mabingwa watetezi wa Copa America Argentina wanaingia kwenye Kombe la Dunia wakiwa miongoni mwa wanaopewa nafasi kubwa baada ya kutoka sare ya kutofungwa kwenye Msimamo wa kufuzu Kombe la Dunia 2022. Odds kubwa za meridianbet

Inashangaza kwamba kikosi cha Lionel Scaloni hakijafungwa katika mechi 35 zilizopita tangu mwaka 2019 wakati Brazil waliwaondoa katika michuano ya Copa America.

Wamebakisha mechi mbili tu kufikia rekodi ya Italia ya michezo 37 ambayo iliwekwa kati ya Oktoba 2018 na Oktoba 2021. Tazama odds bomba na kubwa hapa

Na kuna imani kwamba Argentina hatimaye inaweza kunyanyua Kombe la Dunia kwa mara ya kwanza tangu 1986.

Nahodha Messi anaingia kwenye Kombe la Dunia akiwa katika kiwango kizuri akiwa amefunga mabao 12 na kusaidia mengine 14 kutokana na mechi 18 alizocheza katika michuano yote akiwa na Paris Saint-Germain. Beti na meridianbet wana odds bomba

 

Messi Kuiongoza Argentina Kutwaa Ubingwa WC 2022

Anaungana na washambuliaji wenzake Dybala, ambaye amefunga mabao saba katika mechi 11 tangu ajiunge na Roma majira ya joto.

Mchezaji nyota wa Inter Milan Martinez ana mabao nane, huku nyota wa Manchester City Alvarez akifunga mabao saba chini ya ukufunzi wa Pep Guardiola.

Alvarez ni mmoja wa wachezaji watano wa Premier League waliojumuishwa kwenye kikosi cha Argentina.

Mlinda mlango wa Aston Villa Emiliano Martinez ametajwa pamoja na beki wa kati wa Tottenham Cristian Romero, mlinzi wa Manchester United Lisandro Martinez na kiungo wa Brighton Alexis Mac Allister. Odds bomba zinapatika hapa.

Beki wa zamani wa City Nicolas Otamendi na mchezaji wa United Angel Di Maria pia wamejumuishwa kwenye kikosi.

Vile vile ni mlinzi wa zamani wa Spurs Juan Foyth ambaye amejipanga upya tangu alipoondoka kaskazini mwa London kuelekea Villarreal.

Gwiji wa Uingereza John Barnes ameipa nafasi Argentina kutwaa Kombe la Dunia huku akiunga mkono Messi kushinda Kiatu cha Dhahabu.

Acha ujumbe