Klabu za Inter na Roma zinaungana na Manchester United na Arsenal wanaotajwa kuwa wanavutiwa na kiungo wa Atletico Madrid Thomas Partey.
Kwa mujibu wa chapisho la Mundo Deportivo, raia huyu wa ghana amezivutia klabu kadhaa za Italia na Uingereza.
Nyota huyu ana mkataba na klabu ya Atletico hadi Juni mwaka 2023. Mkataba wake unatajwa kuwa na dau la kumnunua la Euro milioni 50 lakini mazungumzo zaidi yanaweza kukamilisha biashara yake.
Kiungo huyu alitokea kwenye klabu ya vijana ya Atletico Madrud na mpaka sasa amecheza mechi 35 msimu huu, na kuchangia magoli 3 na asisti 1.
Mundo Deportivo wanasisitiza kuwa Inter Milan walihitaji kumsajili nyota huyu mapema zaidi na walishafanya majaribio kadhaa kukamilisha uhamisho wake, huku vilabu vya Manchester United, Roma na Arsenoal wakiunga tela hivi karibuni kuonesha kuvutiwa naye.


Mariam mtandama
Asante meridianbet
Furahav
Thomas yuko vizuri
Omary lukumbi
Thomas partey ni mchezaj mzr tuu