Manchester United wanahitaji kujiandaa kuwa tayari kutumia £90m kama wakihitaji kuinasa saini ya Jack Grealish kutoka Aston Villa.
Nyota huyu mwenye uraia wa Uingereza bado anaendelea kuhusishwa na uhamisho wa kutimba Old Trafford licha ya United kuamua kumsajili Donny van de Beek i msimu wa joto uliopita.
Grealish amekuwa kwenye fomu nzuri sana pale Villa msimu huu, akiwa ametoa jumla ya asisti na magoli 15 kwa pamoja kwenye mechi zake 15 za Ligi ya Uingereza alizocheza msimu huu.

Aston Villa wanatambua na kukubaliana na ukweli kuwa nyota huyu wa miaka 25 atashawishiwa kwenda sehemu nyingine, lakini vyanzo vinasema watahitaji kuruka kiunzi cha dau kubwa kuinasa saini yake.
Grealish alisaini mkataba mpya na Villa mwezi Septemba mwaka jana, na mkataba wake wa sasa utashuhudia akiendelea kuitumikia klabu hiyo hadi mwisho wa kampeni ya 2024-25, ikiwa hatakamilisha uhamisho wowote.
Paul Dyabala kutoka Juventus pia anatajwa kuwa kwenye malengo ya Manchester United, hata hivyo mpango huu wa Ole Gunnar unaonekana kutokuwa na matumaini ya kufanikiwa katika dirisha hili la Januari.
Ndio, kwetu Mteja ni mfalme. Jiunge sasa na familia ya Meridianbet bila malipo yeyote na sisi tutakuzawadia bonasi ya shilingi 3,500 kama sehemu ya kukukaribisha kwenye familia hii BURE!!!. Unasubiri nini??



Samira
Utd wakaze wamchukue maana ni kiungo bora atasaidia sana
Lydia Emmanuel Magoti
Wakikaza nakititachapesa kikikamilika Amna shida tutamnyaka tuuu kilakitu pesa tuuu hapo
Shakila mrope
Yetu macho tuangalie
Rahmal
Nice
Adelta
Watafute pesa kila kitu kitakuwa sawa
Gabriel
Jaman man u hawanahela msimu huu hatar
Magdalena
Mtihan sana pesa ndefu
warda
Kwa Man u watampata tu
Sania
Hapo mchezo pesa
Tatu
Wamwage pesa
Sabrina
Man u wajipange wamchukue jeshii huyo
Caroline
Pesa madafu
Dorophina
Jack yupo vizuri tatizo man u mfuko wao unasemaje
Saupha mohamed
Mpango pesa tu
Angelina
Man u lazima wamnase
Issa
Graelish ni moto sana
Hopemwaikuka
Man atushndw jambo
Sarah
Mambo yapesa tu hapo