Yanga katika kujiweka salama na fitna za soka nchini, wameweka Masharti Mawili katika makubaliano ya kusitisha mkataba na kiungo wake Carlos Carlinhos anayedai kutopenda mazoezi magumu.
Sharti la kwanza ni endapo atakwenda na kisha kurudi ndani ya misimu minne kutoka sasa Yanga ivune pesa katika dili hilo wakitaka walipwe dola 200,000 (zaidi ya Sh 480milioni).
Inaelezwa hatua hiyo ni kukwepa janja janja ya Simba au Azam kuwageuka na kumsainisha kwa urahisi, pia kama ikitokea hivyo basi Yanga wavune pesa ya maana katika muda huo.
Tayari mabosi wa Yanga wameshatoa baraka kwa Ofisi ya Katibu mkuu kumalizana na kiungo huyo. Pia wakitaka atafutwe kiungo wa maana kama Carlinhos ili kuziba nafasi yake na inelezwa huenda akawa mzawa.
MAANA KAMILI YA USHINDI KATIKA KASINO ZA MERIDIANBETI NI PAMOJA NA MCHEZO WA PANDA PANDA.
Hii ndiyo burudani yenye ushindi! Ingia kwenye kasino ya Meridianbet kufukuzia ushindi huu. Cheza sasa Panda Panda na uwe moja ya washindi na Mabingwa.
Dogo anaataka kurudi kwao maisha ya tz yamemshinda
Duuh