Odegaard Awekewa Euro Milioni 60 Na Madrid

Endapo Arsenal watataka kusajili kiungo wao aliyotoka Madrid kwa mkopo, basi watalazimika kutoa Euro Milioni 60 ili waweze kumsajili moja kwa moja!

Odegaard alisajiliwa na Real Madrid januari 2015 akiwa miongoni mwa wachezaji vijana bora ulaya huku akiwa na miaka 16 tu. Katika hatua zake za ukuaji wake Odegaard amepitia timu nyingi kwa mkopo!

Odegaard alitolewa kwa mkopo misimu ya 2018/2019 na 2019/2020, kwenda timu Vitesse Arhem na Real Sociedad ambapo alifaulu sana katika laliga na kuibuka kuwa miongoni mwa wachezaji bora vijana msimu ule, baada ya hapo akaitwa Real Madrid ambapo alijumuishwa kwenye kikosi cha 2020/2021.

Uwepo wa watu kama Kroos na Modric ulimpa ufinyu wa nafasi Odegaard na baada ya hapo akaelekea kwa mkopo Arsenal ambapo toka ajiunge nao January ametoa pasi za magoli 2 na kufunga magoli mawili katika michezo 20.

Amekuwa sehemu ya muhimu katika kikosi cha Arsenal na washika bunduki wanatamani wamsajili moja kwa moja, na Madrid wanataka euro milioni 60 mezani ili wamuachie.

Kuisha kwa msimu wa EPL, kunamanisha mchezaji huyo atarudi tena Madrid ambapo ataendelea kusalia hapo ila Madrid wanaweza kumuuza kutokana na namna ambavyo mchezaji huyo alionesha dharau akiwa anaondoka na suala la kiuchumi linaweza lisimuache salama.


MAANA KAMILI YA USHINDI KATIKA KASINO ZA MERIDIANBETI NI PAMOJA NA MCHEZO WA PANDA PANDA.

Hii ndiyo burudani yenye ushindi! Ingia kwenye kasino ya Meridianbet kufukuzia ushindi huu. Cheza sasa Panda Panda na uwe moja ya washindi na Mabingwa.

Gomes, Gomes : Sitafanya Usajili wa Kutisha., Meridianbet

CHEZA HAPA

2 Komentara

    Dau kubwa Sana ilo

    Jibu

    Dau nono ilo

    Jibu

Acha ujumbe