Chelsea wameripotiwa kupata pigo kubwa kutokana na taarifa kwamba Ben Chilwell atahitaji kufanyiwa upasuaji wa jeraha la goti.
Baada ya kufanyiwa tathimini wa awali, timu ya madaktari ya Chelsea ilifanya uamuzi wa kusubiri wiki sita ili kuona kama suala hilo linaweza kutatuliwa bila upasuaji.
Hata hivyo, kwa mujibu wa football.london, mchezaji huyo wa kimataifa wa Uingereza sasa ameambiwa kwamba atatakiwa kuwa nje nje ya uwanja kwa muda mrefu.

Ripoti hiyo inadai kuwa tathimini ya pili ilifanyika Jumatatu, hitimisho likiwa kwamba kijana huyo mwenye umri wa miaka 25 atahitajika kufanyiwa upasuaji.
Sakata hili litamfanya ben Chilwell kuwa nje kwa muda wote uliosalia wa msimu, na hivyo kumlazimu kocha mkuu wa Chelsea Thomas Tuchel kutafuta mbadala wake wakati wa usajili wa dirisha dogo la usajili la mwezi Januari.
Nani hapendi kuwa bingwa na kujishindia mkwanja wa kusahato kuelekea katika sikukuu wiki hii. Mchezo wa Ocean Call kutoka kasino maridhawa za meridianbettz unakupa kila sababu ya kuifanya siku kuu yako kuwa ya kuvutia zaidi.


