Barcelona wamekamilisha usajiri wa winger Ferran Torres kutoka Manchester City ambapo leo ndio ametangazwa rasmi kuwa mchezaji wa barcelona mpaka mwaka 2027.
Barcelona wamemsainisha mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 21 mkataba mpaka mwaka 2027 huku kukiwa na kipengere cha kuvunja makataba wake kwa €1 billion na mchezo wake wa kwanza kuvaa jezi ya Barc utakuwa dhidi ya Linares Deportivo tarehe 5 Januari 2022 kwenye michuano ya Copa del Rey.

Tatizo la kifedha walilonalo klabu ya Barc wameliweka sawa, huku deni lao likiongezeka kufikia €1 billion baada ya kuondoka kwa Lionel Messi na Antoine Griezmann majira ya kiangazi yaliyopita.
Kuondoka kwa Griezmann na kustaafu kwa Sergio Aguero kutokana na tatizo la moyo, kumetoa mwanya kwa Barcelona kuweza kuwasajiri Ferran Torres na Dani Alves, huku La Liga wakiweka sheria ya matumizi ya €97milion kwa msimu ikijumuisha mishahara na pesa zinazotumika kununua wachezaji.
Barcelona wameruhusiwa kutumia asilimia 25% ya kiasi cha pesa wanachookoa kutoka kwenye mishahara na wanachouza wachezaji wao.
Unaanzaje siku yako katika msimu huu wa sikukuu, mchongo upo meridianbet kasino. Sloti pendwa ya Sahara Richies inaweza kukufanya ukawa milionea katika kufunga mwaka huu, Jiunge na ufurahie kasino maridhawa kutoka nyumba ya mabingwa.

CHEZA HAPA

