Aliyekuwa kocha mkuu wa klabu ya Bristol city inayoshiriki ligi daraja la kwanza nchini Uingereza, Lee Johnson amesimamishwa kazi kama kocha katika klabu hiyo.
Taarifa hizo zimethibitishwa na website ya klabu hiyo jana, muda mchache baada ya kupoteza mchezo wao dhidi ya Nottingham forest kwa bao moja kwa sifuri.
Kocha msaidizi Dean Holden amepewa mikoba ya kuwa mwangalizi katika timu hiyo mpaka kocha mkuu mpya atakapo patikana.
Bristol city imeshindwa kupata matokeo ya ushindi katika mechi zao 5 zilizopita ikiambulia vipigo mara 4 na kupata suluhu katika mchezo 1.
Bristol city inashika nafasi ya 12 katika msimamo ikiwa na alama 55, alama 10 kutoka katika nafasi ya kushuka daraja.
“Tunatambua nguvu na akili alizowekeza Lee katika miaka yote minne na nusu kufanya klabu hii iendelee, tunamshukuru kwa kazi yote akiyofanya, tutaendelea kukumbuka muda wote mzuri tulio kuwa pamoja.
“Ingawa, mafanikio katika mpira yanapimwa kwa matokeo na nafasi katika ligi, kamati inaamini mabadiliko katikika uongozi yanahitajika katika klabu ya Bristol City.” Mark Ashton ambaye ndiye mtendaji mkuu amezungumza.
Dorophina
Wanakazi ya kutafuta kocha bora ili aweze kuipandisha daraja timu
Ester jackson
Pole sana kocha Johnson sio kwamba umefanya vibaya katika timu ila ni mabadiliko ya kawaida na sheria kama hutaleta maendeleo katika timu basis utahitajika kuondolewa hizo ndio changamoto utapata sehemu nyingine ili umbambane vilivyo
Zeiyana
Ingawa mafanikio katika mpira yanapimwa kwa mtokea lee johnson akuna matokea yoyote yaliopatikana bristol city ni bola waangalie upande mwengine tu
isha
Pole sana bwana lee johnson kwa kufukuzwa hapo klabu lakini wala usiwaze kuna maisha mengine
Aziza mushi
Pole sana kochaa utapata timu nyingine
Khadija
Pole sana kocha johnson#meridianbettz
Genia Sikaluzwe
Pole Sana Johnson ili usijali baada ya hapo maisha mengine yata endelea
Mariam mtandama
Pole sana kocha
Angelina
Pole yake akatafute maisha mengine
Lydia Emmanuel Magoti
Duu pole yakee
Rehema
Duuh! Jaman pole yake
Caroline
Pole yake
felister
sad news
Mwanahamisi
Pole yake
nasra
Pole aisee
Shafii
Hatuwezi kusema ni mwalimu mbaya Laa hasha ila inawezekana hakuendana na falsafa ya clubuni hapo ila sio jambo La kukata tamaa akajaribu bahati yake club itakayo hitaji kandarasi take.
Hamidu
Asante kwa update za michezo#meridianbettz
Sadick
Watalaamu wanasema ukiona mambo ktk Kampuni hayaendi badili meneja hivyo Bristol wamezingatia ushauri huu wa wahenga.Tusubri na kuona#meridianbettz
Johnmary joel
Pole sana ila wanakazi wakutafuta kocha mzuri hatakae weza kuongoza timu hiyo ili iweze kupanda daraja#meridianbett
Fatuma kasomo
Pole usijali maisha popote
farida ahmadi
Pole sana kocha Jonson ila kambi popote
Sabrina
Maoni:Lee Johnson utapata timu nyingine
Njiku
Johnson anaonekana kuwa kocha mzuri ila uongozi wa klabu ya Bristol city inaharaka na mafanikio nia ya kucheze EPL ndio tatizo kocha huyo ndani ya miaka yote aliokuwa hapo hakufanikisha hilo
Edgar
Pole sana sema mambo mengine hayataki haraka jaman..
Magdalena
Wangempa muda wa kujua namna ya kurekebisha matatzo kumfungashia virago si suruhisho
Frank Patrick
So sad but ako na nafasi ya kuifundisha team nyingine na akaipa mafanikio tu
Samiah
Atafute maisha mengine
Povel
Duh majanga kwl
Devotha
Pole sana Lee Johnson utapata timu ingine
Furahav
Ukocha unakazi sana.
Amiri Kayera
Kocha anaajiliw ili atimuliw
Saupha mohamed
God news
Omary lukumbi
Duuu hyo si jambo la kushangaza ila atapata tuu club nyingine akafundisha
Theckla
Soka Lina changamoto zake Nina Imani kwakuwa ni kazi yake atapata timu nyingine
Latifa juma mohamed
Duuh pole Sana kocha lkn kuchanika kwa jamvi sio mwisho wa maongezi ,imani kubwa atapata timu nyngine.
David Pere
Bajeti yao ni mbovu kocha anaweza kufanya vizuri. Jibu ni hawezi wamemuonea
mwakalosi
katika kazi ambayo ni unpredictable ni hii ukocha tu
Theonestina
Maisha popote Johnson usife moyo.utapata tu timu nyingine
Evaluziga
Pole Sana kocha utapata Tim nyingine
warda
Daaaa Pole Yake#Meridianbettz
tumaini
Maoni:pole sana kocha
Hope mwaikuka
So sad
Mwajuma
Asikate tamaa mlango mmoja ukifugwa mwengine unafunguliwa
Flomena
Tunatambua nguvu na akili alizowekeza Lee katika miaka yote minne na nusu kufanya klabu hii iendelee, tunamshukuru kwa kazi yote akiyofanya, tutaendelea kukumbuka muda wote mzuri tulio kuwa pamoja.
Asia Abdy
Pole yake
Gabriel
Ni kocha mzur tatzo mfumo