Benard Morrison, kiungo mshambuliaji wa Yanga amesema kuwa yupo tayari kwa ajili ya mchezo wao dhidi ya Simba wa Kombe la Shirikisho unaotarajiwa kuchezwa Julai 12, Uwanja wa Taifa.
Morrison alikuwa kwenye mvutano na Yanga kutokana na ishu ya mkataba ambapo kwa sasa inaelezwa kuwa tayari kila kitu kimekamilika kwa mchezaji huyo kipenzi cha mashabiki kurejea uwanjani.

Alirejea mazoezini Julai 2 akiwa ni mwenye furaha na hajasafiri na timu iliyokwenda Mara ambapo kesho itakuwa na mchezo dhidi ya Biashara United.
Morrison amesema:”Nipo na furaha kurejea ndani ya Yanga na mimi ni mchezaji wa Yanga hivyo nitafanya kazi yangu kwa kuwa ninapenda kucheza kwa furaha.
“Kwenye mchezo wetu dhidi ya Simba nipo tayari na nikipata nafasi ya kufunga nitafunga kwani kazi ya mchezaji ni kutimiza majukumu yake,” amesema.
Luc Eymael, Kocha Mkuu wa Yanga amesema kuwa hatamtumia kwenye mchezo wa Biashara United ila Morrison amemwambia yupo tayari kucheza.

“Masuala yake mengine mimi siwezi kuzungumzia ni juu ya uongozi ila mchezaji ameniambia yupo tayari kucheza kwa ajili ya timu na kwenye mchezo wetu dhidi ya Biashara United sitamtumia,” amesema.
Morrison alifunga kwenye mchezo wake wa kwanza wa dabi mbele ya Simba Uwanja wa Taifa Machi 8 wakati Yanga ikishinda bao 1-0.


Evaluziga
Morrison piga Simba hao
David Pere
Swali he atawafunga Tena au watafungwa wao maana Simba wapo Moto sanaa
Theonestina
Mechi itakuwa Kali Sana hiyo
Franky
Ina pendeza sanaa rudi hafanye kweli mpaka kwenye mech sasa
Ernest
Mpira wa Bongo una mambo sana, Haya Yanga bakuli la mshahara wa Morrisson limeshapita??
Hamidu
Morisson ni mchezaji mzuri Sana! Tania zake Kama balotelli..ila asijidanganye kuwafunga Simba safari hii kazi wanayo#meridianbettz
Antony Luseno
Nadhani kurudi kwake sio tishio kwa timu ya simba
Angelina
Hana maajabu simba lazima ishinde
Johnmary joel
Mashabiki wa yanga hii ni habari nzuri#meridianbettt
Fatina mfingi
Simba jeshi
Dorophina
Habari njema kwa mashabiki wa yanga mnyama anarudi tena uwanjani kitawaka siku iyo
Aziza mushi
Simba baba lao ataakirudi aitokei Mara mbali.
Ester jackson
Benard Morrison ni mchezaji mzuri sana kwa kiwango chake ataweza kuwafunga simba hata wachezaji wenyewe wanamjua uwezo wake hapo kama namuona manara anavyo wapangia wachezaji wa simba wakamkwatue miguu ili yanga ifungwe ila kwa uwezo wa mwenyezi mungu yanga itashinda
Mariam mtandama
Asante meridianbet #kwa taarifa
isha
Simba ndio mkali wao hata akirudi nani hatuogopi tunakiwasha tuu uwanjani
Khadija
Itakuwa bonge la mechi simba lazima ichukue ushind#meridianbettz
Tatu
Huyo ni mtoto Mdogo sana kwa simba
Genia Sikaluzwe
Simba lazima washinde na piya wako vizuri
Zeiyana
Habari njema kwa mashabiki wa yanga
Caroline
Yanga damu
Lydia Emmanuel Magoti
Morrison kaz anayo kuikabili wekundu wa msimbazi patakuwa apatoshi hapo
Rehema
Hii mechi itakuwa moto
Mwanahamisi
Hii mechi kabambe
felister
acheni popoganda mpira dk 90 tusubirini iyo siku tuone mbabe atakua nani
Sadick
Hizi drama hazina nafasi ktk ulimwengu wa watu wenye dhamira kutengeneza timu na ligi inayovutia. Haieleweki vema kama masuala yake yametatuliwa au la#meridianbettz
Shafii
Huyo Morrison hata Kama amerudi mazoezini wasimuanzishe kwenye kikosi cha kwanza atawafungisha ni mchezaji wa simba Huyo mamluki tu.
Fatuma kasomo
Tusubir iyo siku ifike
Revina
Lazima arudi huyo mchezaji ni wa Yanga sehemu nyingine akienda anaangaika tu
Njiku
Morrison kiukweli ni mchezaji mzuri kutokana na masilahi ya timu aliamua kusepa kimia kimia na kusaini mikata na simba sports club ila sio mbaya kwa kubanwa na sheria na kurudi katika klabu yake ya zamani ili kumaliza mkataba wake then anaweza kwenda anapotaka ila kwa upande wa game itakuwa kali maana tunajua kuwa wawili hawa wakikutana inakuwa balaa bonge la dabi
Sabrina
Maoni:Mpira dk 90 tunasubiri tuone nan ni nani!
Magdalena
Uyu jamaa simuamini kabisa maacha achelewi kubadilika wawe makini nae
Edgar
Mchezo mkali sana huu utakuwa na kwa bernad kulejea uwanjan Ni moja ya changamoto kwa timu pinzan
Sylvester
Yanga hawajielewi,sijui ni tofauti gani kubwa iliyotokea klabuni na Morrison ila kwa upande wangu Morrison hana nidhamu kabisa.Inawezekana wamemrudisha kambini sababu ya mechi na watani wao wa jadi Simba ila ni upuuzi mtupu.
Issa
Safi arudi awanyooshe tu
Frank Patrick
Mamluki huyu wanamkumbatia wa nini
Povel
Duh habar njema kwa mashabik wa yanga upande wa pil usiempenda kaja ngoj tuone JULY 12
Devotha
Morrison msumbufu sana anaweza kufanya mazoezi siku ya mechi akajificha kocha asimtegemee sana
Amiri Kayera
Saf San jembe
Furahav
Hana lolote huyo.
Omary lukumbi
Hyo mechi.itakua bab kubwa Tanzania itasimama siku hyo maana ina hamasa kubwa kwa mashabiki tanzania.kote na ni daby ya vilabu.kutoka jiji moja la Dar es salaam hii si ya kukosa afe kipa afe beki
Theckla
Bernard merrison ni mchezaji mzuri Sana ila anamaringo Sana binafsi ningependezwa Kama yanga wakamuza tu
mwakalosi
huyu pasua kichwa sana yaani south Africa hawataki kumsikia ila kakutana na wabongo watu wa miyayusho atakaa sawa
Theonestina
Hii itakuwa bonge la mechi kwetu sisi mashabiki wa Simba.yanga lazima afungwe siku iyo
warda
Mmmmm!!!!! Hata haeleweki#Meridianbettz
Salma
Uwenda akaleta mabadiliko
Hope mwaikuka
Kawaida tu
Gabriel
Habar njema sana 👍