Baada ya kumalizana na Alexis Sanchez, sasa Manchester United wamehamia kwa Jesse Lingard. Ripoti zinasema, Man United wapotayari kusikiliza ofa ya timu yeyote inayomuhitaji mchezaji huyo [Lingard].
Lingard ambaye amekuwa na wakati mgumu katika kikosi cha Man United kwa muda sasa, muda wake kusalia katika kikosi cha Ole Gunnar Solskjaer unahesabika. Kuchipukia kwa mshambuliaji machachari Mason Greenwood na mchakato wa kuisaka saini ya Jadon Sancho unaoendelea, ni dhahiri Lingard hana namba tena kunako Old Trafford.

Katika mechi 2 za mwisho alizocheza, Lingard amefunga magoli 2 pekee. Goli la kwanza akilifunga katika mchezo wa mwisho wa Ligi Kuu Uingereza – EPL dhidi ya Leicester City likiwa ndio goli lake la kwanza la Ligi Kuu tangu mwaka 2018. Goli lake la pili ni dhidi ya LASK katika Michuano ya Europa.
Solskjaer bado anasadikika kuwa shabiki wa Lingard kwani aliwahi kumfundisha wakati akiwa timu ya vijana na hata alipokabidhiwa mikoba ya Mourinho kama kocha mkuu wa kikosi cha Manchester United.

Kushuka kwa kiwango na kuwa na mlolongo wa majeruhi kunatajwa kama vichocheo vya Lingard kukosa namba katika kikosi cha Manchester United. Akiwa na umri wa miaka 27 sasa, ni dhahiri Lingard anahitaji kuonesha uwezo wake na kama ataondoka Man United, basi itakuwa ni fursa kwake kufanikisha hilo.
Lingard na Sanchez ni kati ya wachezaji ambao walionekana kama wameshaoneshwa milango ya kutokea kwa kukosa namba katika kikosi cha kwanza na kukumbwa na majeruhi ya mara kwa mara na hivyo kuwa na muda mfupi sana wa kuitumikia timu.

Sanchez amekatisha mkataba wake wa miaka 2 na Manchester United na kujiunga na Inter Millan ambayo alisajiliwa kwa mkopo. Sasa atasalia huko [Inter Millan] kwa mkataba wa miaka mitatu huku United wakimlipa pauni milioni 7.5, na kuokoa pauni milioni 40 ambazo angelipwa kama mshahara wake kwa muda wote uliosalia katika mkataba wake.
Tiketi yako ya kwanza kamwe haiwezi kupoteza ukiwa na Meridianbet. Unarudishiwa 100% ya Tiketi yako ya kwanza.


Caroline
Wanataka Kumuuza Lingard
Sadick
Ni muda kwa Jesse Lingard kuondoka Man U#meridianbettz
felister
popote kambi lingard
felister
popote kambi lingard kila la kheri uendapo
Sauda
Maisha popote Jesse..
Mwajumah
Asante kwa makala
Lydia Emmanuel Magoti
Mbona mnayumba Man U mtaka kumuuza Lingard kwann jamani
Tatu
Aende anapotaka
Furahav
Ila sio mbaya maisha popote.
Fatina mfingi
Mmh Ni sahihi maan wao ndo wanajua uzur wake na ubay wake kwaiyo maamuzi wanayo wao
Issa
Sidhani kama ataondoka lingaad ole ana imani nae
Janeflora malisa
Popote kaz
farida ahmadi
Dah sidhani kama hataondoka lingard
Hope mwaikuka
Kapambane maisha popote
JULIANA
Akapambane mbele
Devotha
Muda wa kuondoka sasa lingard ili mwingine akae kwenye nafasi yako
Sabrina
Duh man u wanamuuza Lingard!
Rose kapinga
Aende tuu akaangalie maisha mengine!!
Gabriel
Itabid akaangalie timu nyingne abadilishe hal ya hewa maana mpk alikuwa anafanana na timu
Omary lukumbi
Lingard bora aende tuu
Neema juma
Maisha popote kijanaa
Zuhura omary kindamba
Usikate tamaa maisha popote
Latifa juma mohamed
Maisha popote hakuna kurudi nyuma.
Shafii
Habari njema kwa makocha.
Ernest
Lingard ni mchezaji mzuri lakini hivi karibuni hakuwa kwenye fomu endapo kama Man U wataamuuza basi ataongeza hasira na juhudi kwenye timu atakayoenda, Nadhani atarudi kwenye fomu
Dorophina
Ni mda wa kusepa sasa lingard kaangalie maisha kwingine
Adelta
Maisha Ni popote aende akapambane
#meridianbettz
Khadija
Maisha kokote nenda tu#meridianbettz
Mwanahamisi
Habari njema kwa makocha
Nasra
Kikubwa uwezo anao
Zeiyana
Lingard hana haja kubaki man Chester ni vizuri kuchezea vilabu vingi ili habadirishe mbinu za makocha wengine
aisha
Jesse nenda popote utakapoona kuwa pana manufaa na wewe
magdalena
lingard alishuka kiwango pale united aende tu kwingine
Amiri Kayera
Kiwango chake kinalud sasa
David Pere
Wenye pesa wajitokeze hasa Kama wake wenye za pale London
Genia Sikaluzwe
Popote kambi
Ester jackson
Wangempa nafasi mana anaonekana kwamba ndio uwezo wake unaaza vizuri sasa ila uwamuzi ni wao zaidi
Samiah
Maisha popote
warda
Lingard nae amepoa sana