Bado hali ni tete kwa winga Willian kufikia makubaliano ya kuendelea kusalia katika kikosi cha Frank Lampard. Suala la mkataba mpya wa Willian bado ni tatizo katika kufanikisha zoezi hili.
Taarifa mbalimbali zinasema Willian anahitaji mkataba wa miaka mitatu ili asalie Chelsea vinginevyo itakuwa ngumu kwake kusalia. Chelsea wamempatia ofa ya mkataba wa miaka miwili pekee na hivyo utofauti wa mwaka mmoja ndio changamoto.

Willian ambaye ameweka wazi adhima yake ya kuendelea kubaki jijini England, bado hajaweka wazi kama atakubaliana na mkataba aliopewa na Chelsea au ataamua kujiunga na timu zingine zilizopo England.
Totenham na Arsenal ni vilabu vilivyopo England na vyote vinahusishwa na kuitaka saini ya Willian ambaye amekuwa na wakati mzuri katika kikosi cha Chelsea kwa takribani miaka 7 sasa.
Wakala wa Willian – Kia Joorabchian amenukuliwa akisema ” Sidhani kama [Willian] amebadilika kwa namna yeyote. Amekuwa mtulivu muda wote. Tulipokua ofa kubwa kutoka Marekani – MLS ambayo ilimtaka ajiunge nao Julai Mosi – lakini amekuwa akihitaji kumaliza msimu na Chelsea na kisha atafanya maamuzi siku moja baada ya mchezo wao wa mwisho”
“Ana ofa mbili kubwa kutoka Ligi Kuu Uingereza – EPL, MLS na mbili za Ulaya . Ataamua baada ya mchezo wa mwisho”
Chelsea wanaonekana kutosumbuka katika hili kwani wamefanya mabadiliko katika sera yao ya mikataba kwa wachezaji wenye umri wa zaidi ya miaka 30. Mwanzoni walikuwa wanaongeza mwaka mmoja na sasa wanaongeza miaka miwili, hawaonekani wakijiongeza zaidi kufikia miaka mitatu kwa wachezaji wenye umri huo – [Willian anamiaka 31].

Lampard alinukuliwa akisema ” naelewa hali ilivyo kwa upande wa klabu. Nina mahusiano mazuri na Willian lakini sijui maamuzi ni yapi. Kama yatatokea wiki ijayo muda wowote kama anavyosema [Willian], basi ni sawa kwa upande wangu vyovyote vile.”
“Nina furaha sana na Willian, amekuwa na mchango mkubwa kwangu na timu kwa ujumla. Utendaji kazi wake na morali kwenye timu ni kitu kikubwa kwangu na timu kwa msimu huu”
“Ni maamuzi yake na nina yaheshimu. Kama akiamua kuondoka , basi Chelsea pia itapaswa kuendelea kutafuta mshambuliaji mwingine”
Chelsea wameshasajili washambuliaji wawili ambao wanaweza kucheza katika nafasi ya Willian. Tayari wamemsajili Timo Werner na Hakim Ziyech, sasa hivi wanapambana kuitafuta saini ya kinda Kai Havertz.

Chelsea watakutana na Bayern Munich katika mechi yao ya marudiano kwenye Michuano ya Ulaya – UEFA wiki hii. Katika mchezo wa kwanza, Bayern alishinda 3-0. Bado Lampard anawakati mgumu hasa wakati huu ambao Pulisic, Azpilicueta, Pedro na Billy Gilmour ni majeruhi. Wakati Jorginho na Marcos Alonso wanatumikia adhabu.
Tiketi yako ya kwanza kamwe haiwezi kupoteza ukiwa na Meridianbet. Unarudishiwa 100% ya Tiketi yako ya kwanza.


Dorophina
Chelsea inabidi wamuongezee mkataba willian mbona ni mchezaji mzuri tu
Lydia Emmanuel Magoti
Wamuongezee tuu mkataba William mbona kiungo mzuri sana
Sauda
Willian yupo vizuri, aongezewe mkataba
Zeiyana
Willian ni mchezaji mzuri sana hila kwa umri wake hakuna timu ambayo itampa mkataba wa mda mrefu kama yeye anavyotaka.
Neema juma
Jamani wamwongezee tu mkataba
David Pere
Wamwache asepe tu maana Arsenal Wana mtaka na yeye anataka kwenda huko
felister
wamuongezee tu
Latifa juma mohamed
Jamani wamuongeze mkataba.
Magdalena
William Ni mahili Sana Chelsea wafanye mpango wamwongezee mkataba aendelee kuitumikia vizuri timu
Ester jackson
Kutokana na uchezaji wake William ni bora Chelsea wamsajili tu hiyo miaka anayo itaka ya miaka mitatu tumeona juhudi anazo zifanya haswa kwenye kipindi hichi kigimu cha kuelekea ubigwa kulikiwa na wachezaji ambao wanauwezo kwa sababu ya majeraha waliyo yapata hawakuwa uwanjani ila yeye alijitahidi sana kama inawezekana wamuongezee tu Mimi kama shabiki wa Chelsea namkubali sana.#meridianbettz
aisha
William ni mchezaji mzuri sana kama nafasi ipo msajilini ili aendelee kukipiga chelsea
Antony Luseno
Sioni sababu ya blues kumpuuzia William waendelee kuwa nae
Isaya massawe
William bado kijana mdogo na nivema akasimamia msimamo wake
Angelina
Goodupdate#meridianbet
marry
bdo mchezaji bora sana apambne zaid
Saupha mohamed
William kijana mdogo sana na anajua sana
Tatu
Chelsea wasipoangalia watamkosa huyo mchezaji
Ernest
Willian bado mchezaji mzuri nadhani anaweza pata timu nzuri zaidi ya Chelsea
Furahav
Wiliam angeenda Arsenal tu.
Salma ngende
Chelsea waspokaza watampoteza
Gabriel
Hapa wakala lazma awe mkwel maana siku zote wakala ndo anayetafuta dili ndie mtu wa kwanza kujua mchezaji anaenda wap?
Fatuma kasomo
Mchezaji mzuri
Hope mwaikuka
Muongezeen buana
Shafii
Tatizo la willian na Chelsea ni swala la mkataba na soka la sasa huwezi kumpa mchezaji mkataba wa mda mrefu wakati umri wake nao hauruhusu.
farida ahmadi
Willium hana maamuzi yake binafsi mwenyewe hivyo akae na timu yake wamalizane
Amiri Kayera
Bado natumai bado ataendelea kubak Chelsea
Mwanahamisi
Mchezaji mzuri
Samiah
Mchezaji mahiri
Theonestina
Wamuongezee mkataba tu
Rehema
Mchezaji mzuri
Nasra
Kiungo bora Sana
Caroline
Willian inabidi awe na msimamo
Mwajumah
Wamuongezee tu mkataba jaman
warda
Mwenzao Anataka kubaki wao hawataki#Meridianbettz
Khadija
Waache ubabaifu wamuongeze tu mkataba#meridianbettz
Sadick
Naamini Willian atakubaliana na sera ya klabu na kuongeza miaka miwili ambayo klabu ipo tayari kumupa#meridianbettz
Devotha
Willian ni kiungo bora mwenye nafasi ya kucheza kwenye timu yoyote hivyo itakua bora zaid kwa Chelsea wakimuongezea mkataba