Kiungo wa klabu ya Liverpool raia wa kimataifa wa Guinnea Naby Keita ambae mkataba wake unamalizika mwishoni mwa msimu huu anatarajiwa kuondoka ndani ya klabu hiyo mwishoni mwa msimu huu kama mchezaji huru.
Klabu ya Liverpool inaelezwa haipo kwenye mazungumzo ya karibu ya kumuongezea mkataba kiungo huyo, Huku ikiwa inataka kuingia sokoni kutafuta kiungo mwingine ili kuboresha safu ya kiungo ya timu hiyo majira ya joto.
Naby Keita amekua akiandamwa na majeraha mar kwa mara kwenye kikosi cha Liverpool hivo kumfanya kukosekana mara kwa mara kwenye michezo ya klabu hiyo, Hivo klabu hiyo inaelezwa kutumia sababu hiyo kama kigezo cha kutukumuongezea mkataba kiungo huyo.
Kiungo Naby Keita inaelezwa atajumuika na wachezaji kadhaa ambao watatemwa na klabu ya Liverpool mwishoni mwa msimu huu, Wachezaji hao ni pamoja na James Milner,pamoja na kiungo Alex Oxlade Chamberlain.
Klabu ya Liverpool ina mpango kumsajili kiungo wa kimataifa wa Ureno Mathheus Nunes ambaye anakiupiga kwenye klabu ya Wolverhampton inayoshiriki ligi kuu ya Uingereza, Kiungo huyo inaelezwa ndio sababu ya Naby Keita kutokuongezewa mkataba na klabu hiyo kwakua ndio anatazamiwa kua mrithi wake kwenye viunga vya Anfield.

