Papa Bouba Diop Afariki Dunia.

Mchezaji wa zamani wa Fulham, Portsmouth na timu ya taifa ya Senegal – Papa Bouba Diop amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 42.

Diop aliwahi kuvitumikia vilabu mbalimbali vya EPL ikiwemo West Ham United na Birmingham City na alicheza jumla ya michezo 129.

Mashabiki wa Senegal watamkumbuka Papa Bouba Diop kwa kufunga goli la pekee katika mchezo dhidi ya Ufaransa katika mashindano ya Kombe la Dunia mwaka 2002.

Diop Alipokuwa akiitumikia West Ham United.

Kupitia ukurasa wa Fifa, imeandikwa “Uliwahi kuwashujaa wa Kombe la Dunia, utabaki kuwa shujaa wa Kombe la Dunia.”

Ukurasa wa twitter wa timu ya Fulham wameandika ” klabu inahuzunika. Pumzika kwa amani Wardrobe”

Diop Alipokuwa akiitumikia timu ya Taifa ya Senegal.

Diop aliisaidia Senegal kufika hatua ya robo fainali kwenye Kombe la Dunia 2002 na alicheza mashindano ya Afcon mara 4 yakiwemo mashindano ya mwaka 2002 ambapo Senegal walimaliza nafasi ya pili na mwaka 2013, Papa Bouba Diop alistaafu kucheza soka.

Rais wa Senegal  – Macky Sall amesema “kifo cha Diop ni pengo kubwa kwa Senegal.”


FURAHIA MUZIKI MTANDAONI HUKU UKITENGEZA MKWANJA!!

Mchezo wa Astro Legend unakupatia burudani ya muziki kupitia kasino ya mtandaoni ya Meridianbet. Utaburudika huku ukiendelea kutengeza mkwanja mrefu, jiunge sasa na uwe miongoni mwa mabingwa!!

INGIA MCHEZONI

11 Komentara

    Mungu hamraze mahara pema peponi papa bouba

    Jibu

    Pumzika kwa amani

    Jibu

    R.I.P

    Jibu

    Mungu ampungudhie adhabu ya kabri

    Jibu

    R.i.p bouba

    Jibu

    Legend has gone

    Jibu

    Rest well champ

    Jibu

    Duh pumzika kwa amani

    Jibu

    Pumnzika Kwan amani

    Jibu

    Pumzika kwa amani

    Jibu

    R.I.P

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.