Simba SC wanajiandaa kwa Kituo kinachofuata ndani ya Ligi Kuu Bara ikiwa ni mchezo dhidi ya KenGold unaotarajiwa kuchezwa Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi ikiwa ni mzunguko wa pili.

Mchezo wake wa mwisho kwenye ligi ilikuwa dhidi ya Singida Black Stars uliochezwa Uwanja wa KMC Complex na mwisho ubao ulisoma mnyama 1-0 Singida Black Stars. Bao pekee la ushindi katika mchezo huo lilifungwa na mshambuliaji Steven Mukwala ambaye alitumia pasi ya Jean Ahoua kiungo mshambuliaji mwenye jumla ya pasi 8 ndani ya ligi namba nne kwa ubora.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa

KenGold kwenye msimamo wa ligi ipo nafasi ya 16 ikiwa na pointi 16 baada ya kucheza mechi 28 msinu wa 2024/25. Inakutana na Simba SC iliyo nafasi ya pili pointi 72 baada ya mechi 27 ikiwa inapambania kutwaa ubingwa mbele ya Yanga SC ambao ni vinara wenye pointi 73.
Kwa upande wa mabao Simba SC imefunga mabao 63 inakutana na KenGold ambayo imefunga jumla ya mabao 22.

