Mousa Camara Kutemwa Simba

Camara kipa namba moja wa Simba SC anatajwa kuwa kwenye hesabu za kukutana na Thank You ndani ya kikosi hicho kinachonolewa na Kocha Mkuu,Fadlu Davids.

Mousa Camara Kutemwa Simba

Camara ni chaguo la kwanza ndani ya Simba SC ambayo ipo kwenye maandalizi kuelekea mchezo wa Ligi Kuu Bara dhidi ya KenGold unaotarajiwa kuchezwa Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi, Juni 18.

Taarifa zinaeleza kuwa kipa huyo ambaye amekaa langoni kwenye mechi 25 za ligi akikusanya hati safi 17 akiwa ni kinara kwa makipa ambao hawajafungwa mechi nyingi kiwango chake bado hakijawafurahisha mabosi wa timu hiyo kutokana na makosa ambayo amekuwa akiyafanya.

Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa

Kumekuwa na mgawanyiko ndani ya uongozi wa Simba SC ambapo wapo ambao wanahitaji kipa huyo asepe na wengine wanaamini akipata muda atakuwa bora zaidi.

Mousa Camara Kutemwa Simba

Ikumbukwe kwamba kwenye mchezo dhidi ya Coastal Union mzunguko wa kwanza, Camara alifungwa mabao mawili kutokana na makosa ya safu ya ulinzi na makosa yake kwa kutokuwa kwenye eneo lake mara zote na mchezo dhidi ya Yanga SC alifanya kosa katika kuokoa mpira ambao haukuwa na hatari dakika za lala salama na mwisho akafungwa bao 1-0.

Makosa ambayo kafanya yanatajwa kumuhukumu huku baadhi ya viongozi wakibainisha kwamba kipa huyo alikuwa langoni kwenye mechi za kimataifa mpaka timu inatinga hatua ya fainali.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.