Tetesi za Soka Barani Ulaya.


Tetesi zinasema Barcelona bado haijampatia ofa mpya Lionel Messi, 33, ambaye mkataba wake na klabu hiyo ya Uhispania unakamilika msimu huu wa joto.

Mazungumzo kati ya mshambuliaji wa Barcelona na Ufaransa Ousmane Dembele kuhusu mkataba mpya yanaendelea, huku mkataba wa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 23-ukitarajiwa kumalizika mwaka 2022.

 

Tetesi zinasema kocha wa Paris St-Germain Mauricio Pochettino ana matumaini mshambuliaji wa Ufaransa Kylian Mbappe,22, atakubali kufikia mkataba mpya na klabu hiyo.

Alexandre Lacazette amesema uamuzi kuhusu mkataba mpya Arsenal sio wangu pekee, wakati mkataba wa sasa wa mshambuliaji huyo wa Ufaransa aliye na umri wa miaka 29- ukitarajiwa kukamilika mwaka 2022.

Tetesi zinasema mshambuliaji wa Italia Moise Kean hatarajii kurejea Everton kutoka PSG anakocheza kwa mkopo kutokana na mazingira yalivyo.

Tetesi zinasema kocha wa RB Leipzig Julian Nagelsmann amekaririwa kuwa hajafanya mazungumzo na Bayern Munich juu ya kuchukua nafasi ya Hansi Flick kama kocha wao.

Tetesi zinasema Inter Milan wanataka kumsaini mchezaji Emerson Palmieri,26, kutoka Chelsea.

 

Tetesi zinasema mchezaji wa kimataifa wa Poland na mlinda mlango wa zamani wa Arsenal Wojciech Szczesny, 31, hataondoka Juventus kujiunga na Tottenham msimu huu.

Mkurugenzi wa AC Milan Ricky Massara anasema kuwa anatarajia klabu hiyo itafikia mkataba mpya na mshambuliaji wa Sweden Zlatan Ibrahimovic, 39, na ana imani mlinda mlango wa Italia Gianluigi Donnarumma, 22, na kiungo wa kati wa Uturuki Hakan Calhanoglu, 27, watatia saini mkataba mpya katika klabu hiyo ya Serie A.


Mkwanja Maridhawa na kasino ya 777 Mega Deluxe

Nafasi nyingine kwaajili yako, kasino mpya yenye hadhi ya kipekee inayokupa kila sababu ya kuwa mshindi katika kasino za Meridianbet, anza siku yako na njia rahisi ya kutengeneza mkwanja.

CHEZA HAPA

 

3 Komentara

    Tetesi zinasomeka vizuri

    Jibu

    Ziko bomba tetesi

    Jibu

    Zilinipita sana

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.