Pengine Juni 13 2006 ni siku iliyobeba kumbukumbu mbaya kwa Mkongwe wa soka Zinedine Yazid Zidane ‘Zizzou’, lakini siku hiyo ina kumbukumbu mbaya zaidi kwa mkongwe mwingine wa soka la Italia Marco Materazzi, nitakwambia kwa nini.
Siku hiyo ni siku ambayo ulimwengu wa soka ulishuhudia mchezo wa fainali ya kukata na shoka kati ya miamba miwili ,yani Ufaransa dhidi ya Italia. Ufaransa waliingia wakiwa wamepewa nafasi ya kushinda mechi hiyo na kuubeba ubingwa huo hasa kutokana na ukubwa wa majina waliyokua nayo katika kikosi. Hivi unatokaje mbele ya timu yenye Thiery Henry, Eric Abidal na William Gallas? Kama unafikiri haiwezekani, niambie utafikiria nini baada ya kuambiwa kikosi hicho pia kilikuwa na Claude Makelele, Frolent Malouda, Frank Ribery na fundi mwenyewe Zinedine Zidane! Ufaransa walikamilika bwana.
Lakini kama unavyojua, katika soka halitokei jambo kabla halijatokea. Ufaransa waliambulia kupata sare ya kufungana goli moja kwa moja, na baadae wakapoteza katika changamoto ya mikwaju ya penati mbele ya ‘watukutu’ wakina Cannavaro, Grosso, Andrea Pirlo na wenzao wa Italia.
Zidane hawezi kuisahau hii siku kwa kuwa ndiyo ilikua siku aliyocheza mechi yake ya mwisho akiwa na timu ya taifa ya Ufaransa. Kama hilo halitoshi kumfanya asiisahau hii siku basi ataikumbuka kwa kuwa ni siku ambayo licha ya kuwa walipoteza dhidi ya wapinzani wao yeye alipewa heshima ya kutunukiwa tuzo ya mchezaji bora wa mashindano. Hilo nalo likimfanya asiikumbuke siku hiyo basi atajiwe jina ‘Materazzi’, hapo kumbukumbu zake zote juu ya hii siku zitarudi mujarabu kabisa!
Zinedine Zidane, dunia ikiwa inamtambua kama mchezaji bora kabisa tena aliyepata fursa ya kutunukiwa tuzo ya FIFA ya mchezaji bora wa dunia mara tatu, yani mwaka 1998, 2000 na 2003. Siku hiyo alijikuta akifanya kitu cha ajabu na cha fedheha kubwa katika mchezo wa soka kwa kumtundika kichwa cha kifuani mlinzi wa timu ya taifa ya Italia Marco Materazzi baada ya kutokea vita ya maneno baina yao.
Sio watazamaji tu walioshtushwa na kitendo kile, hata mwalimu wa kikosi cha Ufaransa wakati huo Raymond Domenech na benchi lake la ufundi hawakuamini sio tu kutokea kwa tukio hilo, lakini pia kufanywa na ‘Zizzou’ tena akiwa nahodha wa kikosi chao. Zidane ni mchezaji aliyeheshimika sana katika ulimwengu wa soka, tukio la namna ile kutoka kwake halikutegemewa na yeyote yule.
Mwisho ule kwa Zidane ulikua wa kukarahisha sana, kuhitimisha safari yake ya kulitumikia taifa la Ufaransa kwa kutolewa nje ya uwanja kwa aibu ya adhabu ya kadi nyekundu sio kitu ambacho atakisahau kamwe. Na kingine kibaya ni kuwa matokeo ya kitendo kile yakaigharimu timu ikakosa ubingwa mbele ya Italia.
Pamoja na kuwa mashabiki wa soka nchini Ufaransa walionesha kumsamehe na kumuunga mkono nguli huyo, sidhani kama yeye binafsi tayari amejisamehe kwa maamuzi yale. Pengine Zizzou angemaliza dakika zile za mwisho mwisho angefanikiwa kufanya jambo na kufanya mechi ile isifike hatua ya ‘matuta’, lakini hayo yamekwishapita. Historia imeshaandikwa na hakuna anaeweza kuibadili.
Zidane amewahi kunukuliwa mara kadhaa na vyombo mbalimbali vya habari akisema kuwa anaumizwa na tukio lile, lakini mara zote hizo amekataa kumuomba msamaha Materazzi. Alikwishawaomba msamaha wachezaji wenzake wa Ufaransa, mashabiki na ulimwengu mzima wa soka kwa kile kilichotokea. Lakini kuliko kumuomba msamaha Materazzi ni bora afe!
Inasemekana kuwa Materazzi alimtukania Zidane mama yake na ndiyo sababu Zizzou alipatwa na hasira hali iliyopeleka kufanya tukio lile, lakini yeye Materazzi alisema kuwa hakumtukania mama bali dada yake. Kwa hiyo jambo moja liko bayana, Materazzi alimtusi Zidane. Kipo kitu alichokua anakitafuta kwa Zizzou, na bila shaka alikipata kwani kichwa kile kilitua vyema kabisa mwilini mwake na maumivu aliyoyapata hatokuja kuyasahau. Walisema waswahili, mwana kuyataka mwana kuyapata.
Asia Abdy
Mnatujuza mengi #meridian bet
Mwajuma
Zidane ni mchezaji niliekuwa na mkubalia sana
Samiah
Asanteeee meridian kwa taarifa
Fatina
Asanteh kwa taarifa meridian tunawapat vizur
David pere
Hii ndosi itakumbukwa milele
Zeiyana iddi
Asante meridianbet kwa kutupatia taarifa
Dorophina
Mnatupatia wateja wenu kile tunachostahili
Neema hassan
Asnte kwa taarifa meridian mko juu..
mathayo sonje
pale mzee mzima zizu alikua na jazba akakosa hata uchezaji bora, maana alilimwa kadi nyekundu ikionesha utovu wa nidhamu. ila meridian kwa kuchimbua mambo hata hili?
Aziza
Meridian mnatupatia kweli asnten sana
Gabriel
Naikumbuka hii gemu ilinitoa machozi
Theckla
Kumtusi mtu si Jambo zuri na mtu anapokuwa amefanyiwa hivyo yuko radhi kutanya chochote kuridhisha nafsi yake kwa hy zidane alikuwa sahihi kufanya vile ili kupunguza Asira alizokuwa nazo.
Ester jackson
Asante kwa taarifa kama hii
Lombo
zidane alikuwa mtata hukiingia kweny anga zake
Adelta
Nakumbuka hii gemu iliniuma sana
Ester mmakasa
Mimi nilikuwa siyajui yote haya lakini baada ya kujiunga na app ya meridianbet ,sipitwi na habari yoyote.
Hopemwaikux
Habar hii ni nzur sana kwetu mashabik axanten
Neema juma
Kwelii aise mwana kuyataka mwana kuyapata
geniaskaluzwe8
zidane mtu mbaya
felister
hasira hasara utakiw kuruhusu hasira ikutawale
Lydia Emmanuel Magoti
Zidane alikuwa ataki masihara alikuwa Atari sana uyo
Jenifer
Asanten sana kwa taarifa meridianbet
winfrida
kwakweli zzizou alitia huruma
Salma
Mtoto akililia wembe muache umkate
Nasra
Asantee kwa taarifa nzuri
Povel
Zizzou pale alizinguwah kwl hakutumiah busara za kiutuuzima wake na hta burudan ya michezo ilipunguwah kiasi fulan Asante meridian kwa habar za kisport
aisha
ahsanteni meridian bet kwa taarifa njema
christopher
Zidane akaona aachane kabisa na soka baada ya hyo game
Tahiya
Asante kwa kutujuza
Amani
Mko vizuri na huduma zenu
David pere
Mnatisha Sana jamanii
Mwanahamisi
Asante kwa taarifa
Ernest
Mpira una mambo mengi sana, lakini hapa Zidane kuwa alipitia kucheza mpira wa chandimu.
Shafii
Zidane akufanya kitendo Cha kinizam
Hamidu
Nakumbuka fundi zizzou alifanya yake.
Mwoshi wa siku akalimwa red Card najua zilikuwa figisu za materazi.
Rehema
Asante kwa taarifa meridianbet
Antony Luseno
Kupewa nyekundu kwa Zizou kuliikosesha France ubingwa kwa asilimia Fulani
Agness
Asantee meridian kwa taarifa
Rehema Dickson
Kwakwel meridian mnanipa habari nzuri sana tangu nijiunge na nyie kwakwl habari zote zinazohusiana na mpira nazipata kwenu nawapongeza kwa habari nzuri
Frank patrick
Icon zizzou
SADICK
Lilikuwa tukio la aibu sana. Asante kutukumbusha #meridianbettz
Emmy cleopa
Ahsante meridian kwa taarifa
Furahav
Mmh hilo sikichwa bali ndosi.
Sadick
Ulikuwa usiku wa kukumbukwa sana. Ni watu wachache hufikiria mara mbili kabla ya kutenda wanapopata hasira,ndio maana leo tujiuliza kwanini alifanya hivyo bila kufikiria dhamana aliyokuwa nayo!. Hata hivyo maisha yanatakiwa kuendelea. Asante kutukumbusha kisa hiki#meridianbettz