UEFA wametoa kiasi cha paundi milioni 236.5 kwa ajili ya mashirikisho ya soka 55 ambayo ni washirika wake ili waweze kupata ahueni katika kipindi hiki kigumu.
Fedha hizi zimepatikana kutoka kwenye programu ya UEFA ya msaada ya HatTrick. Program hii ilianzishwa mwaka 2004 ikiwa na lengo la kuboresha mendeleo ya soka Ulaya.
Kutokana na mpangilio wa program hii, kila shirikisho mwanachama ikiwa ni pamoja na FIGC wataweza kutumia pesa hizo kwa kadri wanavyoona inafaa katika kujikwamua na changaoto kadhaa wakati huu.
Kupitia tovuti ya UEFA, raisi wa mamlaka hii kubwa ya soka Ulaya Aleksander Ceferin amesema kuwa soka limepata changamoto kubwa iliyoletwa na janga la Corona. UEFA haijataka kuwaacha washirika wake wapambane peke yao na wameamua kutoa msaada kadri wanavyoweza.
Kupitia Raisi, wamebainisha kuwa nia yao ni kutoa kiasi cha angalau paundi milioni 4.3 kwa kila shirikisho la soka inayolipwa kwa msimu uliosalia na msimu ujao kuwasaidia washirika kuziba mapengo katika kuboresha hali ya soka.


Daniel
WOW
Kenani
Ni vizur kuboresha soka na burudani
Theckla
Asanteni kwa habari nzuri za kimichezo