Virgil Van Dijk Afunguka kuhusu Klopp.

Beki wa klabu ya Liverpool na timu ya taifa ya Uholanzi Virgil Van Dijk amefunguka namna ambavyo kocha wa klabu hiyo Jurgen Klopp anvyokua mkali kwenye vyumba vya kubadilishia nguo.virgil van dijkKlabu ya Liverpool ambayo imeanza vibaya sana kwenye ligi kuu ya Uingereza baada ya kupata ushindi kwenye mechi tatu tu msimu huu kwenye ligi hiyo huku wakiwa nafasi ya nane ya msimamo huku wamevuna alama 16 tu ikiwa ni rekodi mbovu sana kwenye historia ya klabu hiyo kwa miaja nitano ya hivi karibuni.

Virgil van Dijk ameeleza namna ambavyo kocha wa timu hiyo anakua mkali pale ambapo wanakua wanafanya vibaya kwenye vyumba vya kubadilishia jmambo ambalo limekua likiwakera wachezaji pamoja na yeye lakini hufanya hivo ili kuwaboresha na kufanya vizuri zaidi.virgil van dijk“Kwa hivyo, ninafurahiya sana hilo kwa njia inanisaidia binafsi. Nilikua nikaribu kwenda moja kwa moja na alikua akinifokea na kusema tulipaswa kufanya vizuri zaidi” Anaeleza beki huyo.

Virgil van Dijk ameeleza kocha huyo amekua mkali sana pale ambapo wamekua wakipoteza mchezo ama kufanya vibaya ila beki huyo amesema hua inawasaidia kufanya vizuri zaidi kwasababu hua hawapendi kufokewa na hiyo inawafanya kufanya vizuri ili kuepuka hasira za mwalimu huyo.

Acha ujumbe