Wesley Fofana Anaitaka Chelsea.

Mchezaji wa klabu ya Leicester city inayoshiriki ligi kuu ya uingereza Wesley Fofana ameendelea kusisitiza juu ya nia yake ya kujiunga na klabu ya Chelsea.

Beki huyo mwenye miaka 21 mzaliwa wa Ufaransa mhitimu wa akademi ya Saint Etienne anatamani kwenda klabu ya Chelsea na kwake anaiona kama klabu ya ndoto zake.

Chelsea waliamua kumgeukia beki huyo ni baada ya kukosa beki mwingine raia wa Ufaransa Julias Kounde alietimmkia klabu ya Fc Barcelona ya nchini Hispania.

klabu ya Chelsea wamepeleka ofa tofauti tofauti kwa klabu ya Leicester City inayommiliki mchezaji huyo lakini zote zimepigwa chini mpaka ofa ya mwisho ya paundi milioni 70 nayo imepigwa chini. Lakini upande wa mchezaji inaonekana kuhitaji dili hilo litimie ili aweze kujiunga na klabu ya Chelsea.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.