Nyota wa klabu ya AC Milan mbabe na mwenye vituko Zlatan Ibrahimovic atakuwa nje ya uwanja kutokana na upasuaji ambao amefanyiwa na inatajiwa utamuweka nje kwa mwaka huu mzima.
Zlatan Ibrahimovic jumapili iliyopita alifanikiwa kushinda ubingwa wa ligi kuu ya Italia Serie A akiwa na klabu ya AC Milan, na ukiwa ubingwa wake wa 14 kwenye maisha yake ya soka lakini mkataba wake na kwenye dimba la san sirro unaisha mwishoni mwa mwezi June.
Waraka wa klabu ya AC Milan ambao ulichapishwa kwenye wavuti wa klabu hiyo, “AC Milan inatangaza kwamba Zlatan Ibrahimovic amefanyiwa upasuaji wa mhuu wake wa kushoto uliodeshwa na Dr Bertrand Sonnery-Cottet, akiwa na mkuregenzi wa matibabu wa klabu Stefano Mazzoni ambaye alihudhuria kwenye hospitali ya Jean Mermoz jijini Lyon.
“Arthroscopy ilikuwa imepangwa kwa muda wakati wakitatua kabisa swala la maungio kutokuwa imara kupitia kutengeneza tena maungio ya ndani ya kifundo cha mguu, ikiwa na upande mmoja wa kiungo hicho na kurekebisha meniscus.
“Oparesheni umekamilikwa kwa mafanikio makubwa na kipindi cha uangalizi chini ya madaktari kinakadiria kitakuwa kati ya miezi saba mpaka nane.”
Ibrahimovic mwezi oktoba mwaka huu anatajia kufikisha miaka 41, je majeruhi haya ndio utakuwa mwisho wake wa maisha ya soka, au ndio atarudi kuja kupigania ili aweze kupata mkataba mpya!
Una Kila sababu ya kufurahia wiki yako na kutengeneza mwaka huu uwe wa faida zaidi katika kasino zetu za mtandaoni za meridianbettz. Mchezo wa Zeus Ancient Fortunes unakuongoza kutekeleza hilo.