Zlatan Ibrahimovic na Olivier Giroud hawajajumuishwa kwenye orodha ya kikosi cha AC Milan kwa ajili mechi ya leo dhidi ya Juventus, wakati Mike Maignan akirejea.
Kwa mujibu wa La Gazzetta dello Sport, kipa huyo wa Ufaransa hayuko fiti kabisa baada ya changamoto ya jeraha la mkono wake.
Mlinda mlango huyo wa zamani wa Lille alipata jeraha kidogo wakati wa mechi ya AC Milan dhidi ya Liverpool pale Anfield mapema wiki hii, lakini amejumuishwa kwenye kikosi kinachosafiri kwenda Turin.
Tiemoue Bakayoko, Rade Krunic na Davide Calabria pia hawapo kikosini kwa sababu ya majeraha.
Ante Rebic atakuwa mshambuliaji pekee wa Milan kwenye Uwanja wa Allianz usiku wa leo na Alexis Saelemaekers, Brahim Diaz na Rafael Leao wakiwa nyuma yake.
Andrea Conti pia anaungana na kikosi huko Turin licha ya kutokuwa sehemu ya mipango ya Pioli msimu huu. Beki wa kulia wa Italia alitumia sehemu ya pili msimu wa 2020-21 kwa mkopo huko Parma.

Kikosi cha AC Milan dhidi ya Juventus
Golikipa: Jungdal, Maignan, Tatarusanu
Walinzi: Ballo-Touré, Conti, Florenzi, Gabbia, Hernandez, Kalulu, Kjaer, Romagnoli, Tomori
Viungo: Bennacer, Castillejo, Diaz, Kessie, Saelemaekers, Tonali
Washambuliaji: Leao, Maldini, Pellegri, Rebic
Unaanzaje siku yako na kuimaliza bila kupitia katika kasino bomba za meridianbettz, mchezo mashuhuri wa Disco Funk unaweza kukufanya uwe mshindi leo hii!


