Pitso Mosimane Aishukuru Yanga kwa Mwaliko

Kocha mshahuri na aliyewai kuvifundisha vilabu vikubwa barani Afrika Pitso Mosimane leo ametoa shukrani zake kwa klabu ya Yanga kwa kumwalika kwenye siku ya wananchi.

Pitso Mosimane ameshawai kufundisha timu ya taifa ya Afrika Kusini, Supersport United, Al Ahly na Mamelodi Sundowns. Pia Mosimane amefanikiwa kuchukua ubingwa wa Afrika mara tatu akiwa na klabu mbili, huku akiweka rekodi bora akiwa na Al Ahly ambapo alifanikiwa kuchukua ubingwa wa afrika mara mbili mfululizo.

‘Safari ya Yanga kwenye siku ya wiki ya mwananchi itakuwa moja ya kumbukumbu kwenye kitabu changu. Sitakuja kuisahau hii wiki na utamaduni wa soka la Tanzania umenivutia sana.

“Kwa raisi, rafiki yangu Eng Hersi, asante sana kwa mwaliko. Nina bahati kwamba mwaliko ulikuwa wakati sahihi. Endelea kufanya kazi yako bora kwenye soka ndani ya jamii yako, hakika unafanya mabadiliko.

‘GSM, wafanyakazi, wachezaji na mashabiki wa Yanga, asante kwa ukaribisho na kunifanya nijisikie niko nyumbani, kiukweli niliufurahia muda wangu. Hadi tutakapokutaba tena.” Aliandika Pitso Mosimane kwenye ukarasa wake wa twitter.

Pitso ndio kocha wa kwanza ambaye siyo raia wa nchi Misri na mweusi kufundisha klabu ya Al Ahly.

 

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.