Pamba Yaitamani Ligi Kuu

UONGOZI wa Pamba FC ya Mwanza umedhamiria kupanda daraja msimu ujao hiyo ni baada ya kusajili nyota wapya kikosini na kuongeza nguvu kwenye benchi la ufundi.

Jana alhamis uongozi ulimtambulisha Kocha wao Mkuu Yusuf Chippo, raia wa Kenya pamoja na benchi zima la ufundi ambalo litaiongoza timu kwa msimu ujao.

Baada ya utambulisho pia Kocha Chippo amefunguka kuwa mipango ya Pamba ni kupanda ligi kuu hivyo hata yeye malengo yake ni kuipandisha timu hiyo ili aweze kuweka rekodi.

Pamba tayari imeanza kutambulisha wachezaji wao ambapo jana ilimshusha aliyekuwa straika wa Simba, Marcel Kaheza pia leo imemshusha pia Peter Mapunda.

Pamba kwa msimu huu itashiriki michuano ya Championship ambapo takriban kwa miaka 20 timu hiyo haijashiriki ligi kuu.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.