Mkurugenzi Mtendaji wa Bayern Munich Oliver Kahn amekiri klabu hiyo ilizingatia kumsajili Cristiano Ronaldo msimu huu wa joto.
Nyota huyo wa Ureno aliweka wazi nia yake ya kuondoka Manchester United ili kutafuta kucheza Ligi ya Mabingwa.

Bayern walikuwa miongoni mwa vilabu kadhaa vikiwemo Chelsea na Atletico Madrid vinavyohusishwa na Ronaldo. Lakini wote waliamua kutomsajili mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 37 na hatimaye alibaki Old Trafford kwa vile United walikuwa na nia ya kuendelea kumshikilia.
Akizungumza na Bild, alisema: “Tulimjadili kwa ufupi Cristiano akiwa Bayern na Dortmund pengine walimjadili pia. Tunaona picha kubwa ya Bundesliga, bila shaka, nyota kama Ronaldo ni jambo muhimu katika kuvutia umakini wa ligi, yeye ni mmoja wa wakubwa zaidi wa miaka kumi iliyopita. Lakini tulipuuza hilo haraka.”

Cristiano amekuwa na nafasi ya kuanza mara moja tu Ligi ya Uingereza msimu huu na hiyo ilikuwa katika kipigo cha aibu cha mabao 4-0 kutoka kwa Brentford mwezi Agosti.

