Lukula Awapongeza Nyota Simba Queens

Kocha Mkuu wa Simba Queens, Charles Lukula amesema kuwa licha ya kufungwa na Mamelodi Sundowns lakini anawapongeza wachezaji wake kutokana na viwango walivyoonyesha.

Simba Queens walipoteza mchezo wao wa hatua ya nusu fainali ya michuano ya Klabu bingwa kwa upande wa wanawake jana baada ya kufungwa bao 1-0 dhidi ya Mamelod Sundowns.

Akizungumza baada ya kumalizika kwa mchezo huo, Lukula alisema: “Nawapongeza sana wachezaji wangu kutokana na viwango walivyoonyesha japo naweza kusema bahati haikuwa kwetu.

“Naweza kusema refa pia hakuwa upande wetu kwani tulipokuwa tunacheza faulo yeye alituadhibu kwa kadi ila kwa wenzetu aliwaambia msirudie.

“Kwa sasa tunaenda kujiandaa kwa ajili ya kupambania nafasi ya tatu hivyo nina imani tutarejea nyumbani na medali.”

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.