Simba Queens: Hatuwaogopi Mamelodi Sundowns

Kocha Mkuu wa kikosi cha Simba Queens, Charles Lukula amesema kuwa hawaiogopi timu ya Mamelodi Sundowns kuelekea kwenye mchezo dhidi yao.

Timu hizo zinakutana leo Jumatano ukiwa ni mchezo wa hatua ya nusu fainali ya michuano ya Klabu bingwa kwa upande wa wanawake.

Lukula amesema: “Mazoezi tuliyofanya ni ya kuhakikisha kwamba tunapata mpira haraka zaidi kutoka kwa wapinzani na nina imani wachezaji wangu watalifanyia kazi hilo.

“Tunajua Mamelodi wamepata pointi zote kwenye hatua ya makundi bila kuruhusu bao lakini sisi hatuwaogopi kwani tumeruhusu bao moja tu kwenye mechi za makundi.

“Tutaingia na mipango yetu kwa kuhakikisha tunavuna hatua hii na kuweka rekodi ya kutinga katika hatua ya fainali.”

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.