Kocha Ibenge Afunguka Kuhusu Uwepo wa Wawakilishi wa Yanga Katika Mechi Zao

Kocha Mkuu wa Azam FC, Florent Ibenge, amesema timu yake haina sababu ya kuficha mbinu zao kuelekea mchezo ujao dhidi ya Yanga SC, akisisitiza kuwa wapinzani wao tayari wanaifahamu vizuri Azam kutokana na mechi nyingi walizocheza msimu huu.

Kocha Ibenge Afunguka Kuhusu Uwepo wa Wawakilishi wa Yanga Katika Mechi Zao

Akizungumza na waandishi wa habari baada ya kumalizika kwa mchezo wao dhidi ya Dodoma jiji fc na Kushida mabao 3-0 aliulizwa kuhusu uwepo wa wawakilishi wa wapinzani kwenye mchezo wake uliopita dhidi ya Dodoma Jiji FC, Ibenge alisema,“Ni jambo la kawaida. Kama ningekuwa katika hali hiyo pia ningekuja kuutazama mchezo wa mpinzani wangu.”

Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa

Kocha Ibenge Afunguka Kuhusu Uwepo wa Wawakilishi wa Yanga Katika Mechi Zao

Kocha huyo ameongeza kuwa Azam FC haina kitu cha kuficha kwa sababu mfumo wao wa uchezaji tayari umeonyeshwa wazi katika mechi kadhaa zilizopita, jambo linalowafanya wapinzani kuwa tayari kuelewa mbinu zao.

Kocha Ibenge Afunguka Kuhusu Uwepo wa Wawakilishi wa Yanga Katika Mechi Zao

Hata hivyo Ibenge alisisitiza kuwa lengo la timu yake ni kuendelea kuimarisha utendaji uwanjani na kuhakikisha wanapata matokeo chanya, bila kuathiriwa na uwepo wa wawakilishi wa timu pinzani. Kwa sasa, Azam FC inajiandaa kwa mchezo huo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara dhidi ya Yanga, huku kocha akisisitiza umuhimu wa umoja na kuzingatia mbinu bora ili kufanikisha ushindi.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.