Mahakama ya Usuluhishi wa Michezo, CAS, imethibitisha rasmi kupokea rufaa kutoka Shirikisho la Soka Senegal (FSF) kupinga uamuzi wa CAF wa kuwanyang’anya ubingwa na kuikabidhi Morocco.
Kupitia taarifa yake, Katibu Mkuu wa CAS, Matthieu Reeb, amewahakikishia wadau wa soka kuwa mchakato huo utashughulikiwa kwa haraka huku ukizingatia haki kwa pande zote zinazohusika.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
“Tumejipanga kikamilifu kushughulikia kesi hii, na tutahakikisha mchakato unaenda kwa kasi iwezekanavyo bila kuathiri misingi ya haki,” alisema Reeb akizungumzia uzito wa shauri hilo.
Senegal waliibuka na ushindi wa mabao 1-0 katika fainali iliyochezwa mwezi Januari, lakini baadaye CAF ilibadili matokeo hayo na kuipa ushindi Morocco kwa mabao 3-0 kwa njia ya ‘forfeit’.
Uamuzi huo wa CAF ulitokana na tukio la wachezaji wa Senegal kugoma na kutoka nje ya uwanja kwa muda wakipinga penalti iliyotolewa kwa upande wa Morocco, jambo lililotafsiriwa kama ukiukwaji wa kanuni za mchezo.
Sasa macho na masikio ya wadau wa soka yanaelekezwa CAS, ambayo inatarajiwa kutoa uamuzi wa mwisho utakaoamua kama kombe hilo litarudi Dakar au litaendelea kubaki Rabat.

