Balotelli Aja Juu "Njoo Mjionee..."

Mshambuliaji wa Brescia, Mario Balotelli amechoshwa na maneno maneno juu yake kama anaendelea na mazoezi au lah!

Inakumbukwa mara Bolotelli aliripotiwa kurejeshwa nyumbani alipowadia mazoezini siku kadhaa zilizopita. Balotelli alinukuliwa akiwaambia waandishi kuwa waandika habari zao kuwa hafanyi mazoezi.

Wakati kasheshe likiendelea kubamba mtaani juu ya jamaa huyu kufanya au kutofanya mazoezi, mshambuliaji huyu ameamua kuja juu na kujibu kuwa yeye anafanya mazoezi na kama vipi “Mje mjionee wenyewe nikifanya mazoezi”

 Mario Balotelli
Mario Balotelli

Staa huyu na klabu yake bado wanaripotiwa kuwa kwenye mgogoro, wakati klabu ikitajwa kuwa haijamruhusu kufanya vipimo vya Corona na pia kutomlipa mshahara wake wa mwezi Machi.

Balottelli aliamua kuchapisha kwenye ukurasa wake wa Instagram kuhusu hali inayoendelea na maswali juu yake.

“Inatosha sasa kuniuliza kuhusu kwenda au kutokwenda mazoezini, ninaenda mazoezini, nimekuwa kule wakati wote, inatosha maswali haya tafadhali.”

“Kama mnataka kuthibitisha mje mjionee wenyewe. Nina vipindi viwili hadi Jumapili, asubuhi na jioni. Njoo hapa utaniona.” -Mario Balotelli

Chapisho lake limeambatana na picha yake akiwa anavuja jasho baada ya mazoezi kadhaa.

39 Komentara

    Balotel ni mkorofi jamani.

    Jibu

    Huyu jamaaa soka lipo mguuni sema tuu nae nidhamu yake na dharau ndo vinamrudisha nyuma

    Jibu

    Yeye no mtu mzima hivyo anajua wajobu wake Kama nilazima afanye mazoezi

    Jibu

    Ballotel anajiamini sana na Mpira anajua ila anajeuri sana huyu

    Jibu

    ni lazima mpaka watu wakuone Kama unafanya mazoezi punguza ukorofi ballotel

    Jibu

    Balotelli n mchezaji mzur ila ukimtibua n mkorofi

    Jibu

    Duh thnks meridian bet tz kwa update zamichezo

    Jibu

    Daaaah hatari Sana hiyo

    Jibu

    Balloteli negativity za watu juu yake zinamuathiri sana

    Jibu

    Daa Balotelli anajua ila ana yumba wapi

    Jibu

    Wanamuonea ila maneno sio mazuri..ballotell fanya kile unachojisikia

    Jibu

    Balotelli yupo vzr#meridianbettz

    Jibu

    Baloteli ni mchezaji mzuri ila mkorofi sn

    Jibu

    Baloteli mchezaji mahiri aache jeuri..

    Jibu

    Simkubal wala nn

    Jibu

    Jamaa anajua sana sema ukorofi upo kwenye damu

    Jibu

    Balotelli ngenge za nini fanya mazoezi tukuone

    Jibu

    Balotel ni mchezaji mzuri Sana Ila sasa ujeuriii.

    Jibu

    Huyu no mcheaji ambaye ni mwehu na ni mjinga namba moja dunian

    Jibu

    Jamaa unazingua sana sisi mashabiki tumechoshwa na drama zako

    Jibu

    Yuko vizuri sana

    Jibu

    Balotelli ni mzinguaji bhn

    Jibu

    Talent player#meridianbettz

    Jibu

    nidhamu yake na dharau ndo vinamrudisha nyuma# meridianbettz

    Jibu

    Anazingua huyu kiande.

    Jibu

    Balotelli mzee wa matukio hata ukifanya haonekani kama hanafanya

    Jibu

    Balotelli ana kiburi sana

    Jibu

    Huyu jamaa kila leo anazungumziwa yeye tu habadiliki hata umri ukimtupa mkono

    Jibu

    Kama ni ndoa tungesema ipo hatarini kuvunjika! Balotelli bado dunia inasubiri kuona kipaji chake halisi#meridianbettz

    Jibu

    Kweli kizuri akikosi kasolo

    Jibu

    Nimzuri ila anazingua

    Jibu

    mmh kama mambo magumu fanya mpango wa kuhama tu ndugu maana marumbano kweny kaz si mazur

    Jibu

    Yuko vizur sana

    Jibu

    Balotelli unaniangusha kwanini uachi utukutu

    Jibu

    Mie namkubali sana huyu jamaa#Meridianbettz

    Jibu

    Nimchezaji mzuri mengine ni madhaifu ya kiubinaadamu

    Jibu

    Baloteli mzuri sema vituko vimezidi uwanjani

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.