Mkude Ukitaka Kuondoka Simba Useme Mapema Tukuage kwa Heshima

Jonas Mkude mpaka kufikia sasa ametoa jasho na damu kuitumikia Simba wangapi walikuja naye saizi wamepoteza dira , wapi Hassan Isihaka ? Wapi Edward Christopher ? Wapi William Lucian Gallas ? na wengine hakika mkude usiondoke kimya kimya kama Ronaldo . Muda mwingine tusiwe tunajitoa ufahamu kila siku Simba inachukua mafundi ndani na nje ya nchi lakini Jonas hajawahi poteza namba , kuondoka sio dhambi ila usemage mapema tukuage kwa heshima kama alivyoagwa Fransisco Totti , kaka Mkude hiyo siku uje na familia yako maana bila wao usingefika hapo , kaka tunahaidi ukisema mapema tutaandaa wimbo wa kukuaga tutaimba kwa pamoja.

Kaka Mkude mpira ni mchezo unaokusanya watu wa kila aina na kila rika wale kina dada wanaishangiliaga Simba kwa mikogo hawatajisikia vizuri kama hutaagwa mzee , kila nikiangalia namna Andres Iniesta alivyokua anaagwa najiuliza kwanini kwako tushindwe ? , jinsi Xavi alivyoagwa Barcelona dah unaweza tokwa na machozi sasa kwanini kwa kijana wetu tushindwe ? . Pale Stadio Olympico siku Fransisco Totti anaagwa uwanja uligubikwa na machozi kila mtu alilia jamaa kustaafu , kaka we tuambie tu ili tuwaonyeshe watu thamani ya kuitumikia timu yako kwa moyo wako wote , hakika tutaujaza uwanja zaidi ya ile mechi ya Ac Vita.

Siku John Terry anaaga pale Stamford Bridge yalijaa mabango makubwa yakionyesha mchango wa JT kaka usihame kwa surprise kaka , yakumbuke maneno machache ya Iniesta “ Katika mkutano huu na waandishi wa habari nataka kusema huu msimu ni wa mwisho ” chumba chote kiligubwiga na machozi , kila mchezaji wa Barcelona alilia kwa uchungu yule Messi ndio ana roho nyepesi hata kwenye mkutano hakuwepo we tuambie kaka usihofu . Kaka tutakuimbia wimbo wa we are heroes tonight sababu wewe ni shujaa wetu , itakua ni makosa duniani na mbinguni kama hatutakuaga kaka sasa jasho na damu ulivyomwaga vitakosa maana kabisa kaka.

Gigi Buffon aliuliza uwanja mzima wa Allianz Stadium kina dada warembo wa Kitaliano waligubwika na machozi hakika ni furaha isiwe na kifani , Allianz Arena ililoa machozi siku Oliver Khan anaagwa sasa kwa nini kwako tushindwe kaka ? , Mkude embu tuambie tuwaoneshe dunia kwamba Tanzania ni nchi ya aina gani na watamani kuja kucheza . Kaka uongeage na Simba waandae utaratibu maalumu wa kukuaga kaka , zitengenezwe jezi maalumu zenye namba 20 pia zitengenezwe skafu zenye jina lako bila kusahau vitambaa na mapambo mengine mengi , lazima tukuage kaka unastahili kuagwa kaka umefanya makubwa mengi .

Jonas Mkude“ Tokea nikiwa kijana mdogo ilikua ni ndoto yangu kuichezea klabu hii kubwa Tanzania Afrika na dunia kwa ujumla , ahsanteni nyote mliokua nami katika safari hii ngumu ya kutimiza ndoto zangu hakika sitasahau siku zote nitawakumbuka , katika ubaya na uzuri wangu hamjawahi kua tofauti na mimi mungu azidi kuwabariki . Popote pale nitakapokwenda ntaitangaza Simba ”

Hisia zote za mashabiki wa Simba , mashabiki wasio wa Simba na wapenda mpira wote nchini zitakua juu yako hakika , kila mitaa na maeneo yote utakayopita utasikia maneno mazuri saana , watu watakushukuru na kulilia.

makala hii imeandaliwa na EZEKIA JOHN KANDONGA.

37 Komentara

    Eeh Afanye hvyo tu

    Jibu

    Thnks meridian bet kwa update za michezo na burudani

    Jibu

    Mmmh kwani mkude anataka kuondoka

    Jibu

    Wanogopa Kama kilichowatokea Yanga kwa Morris

    Jibu

    Mmmm apana maneno yawatu mkude kuondoka Simba hapana labda aseme nimeichoka Simba sio kwavishawishi vyawatu mkude nasimba Moto wakuotea mbali

    Jibu

    No kweli kabisa apewe heshima yake maana amewafanyia mengi Wana msimbazi

    Jibu

    Kweli kabisa mkude akitaka kustaafu atuambie mapema wapenz wa Simba tumuage kwa heshima

    Jibu

    Asante sn meridianbet

    Jibu

    Ni kweli Mana amefanya Mambo makubwa

    Jibu

    Mkude yuko vizuri na anastahiri kupewa heshima yake clubuni hapo

    Jibu

    Mkude unaenda wapi jamani

    Jibu

    Daima mkude ni simba damu hivyo basi hana sababu yoyote ya yeye kutaka kuondoka

    Jibu

    Jmn jembe langu mkude linaenda wp

    Jibu

    Mkude anajua nn anafanya na ndo maana mpaka Leo yupo SimbaSC

    Jibu

    Ni heshima kubwa sana kama mchezaj uliechezea club fulan alafu ukataka kuondoka au kustaafu wakakuaga kwa heshima ina taswira kua walitambua mchango wako mkubwa uliotumikia club kwa kipindi chote cha maisha yako

    Jibu

    Mkude aende wapi tena?

    Jibu

    Wamwache aende tuu

    Jibu

    Izi habari mbna ni zakushtua ivyo Jonas unatak kwenda wapi kijana??

    Jibu

    Ni vizuri amefanya mambo makubwa sana

    Jibu

    Namkubali sana mkude#meridianbettz

    Jibu

    Asante kwa makala

    Jibu

    Mbona sielewi kwani Mkude anataka kusepa AU Ni ushauri tu#Meridianbettz

    Jibu

    Ahsante kwa taarifa

    Jibu

    Asante kwa taarifa

    Jibu

    asiondoke yeye Nani walikuwepo wangapi kwani yeye ndo wakwanza kuichezea Simba…?

    Jibu

    Simba Wana mbwembwe

    Jibu

    jambo zuri

    Jibu

    Wanaogopa kama kilichowatokea yanga

    Jibu

    Kiungo bora Tanzania hakuna kama mkude

    Jibu

    Ni vizuri kumpa heshima yake anayostahili

    Jibu

    Makala nzuri sana, Umegusa kunapo maana imefika wakati kutambua mchango wa wachezaji wetu pindi wanapotaka kustafu au kuhama timu, Salute kwa Mkude

    Jibu

    Duuuuh mkude anaenda wapi tena jamani

    Jibu

    Jonas Mkude namukumbuka kwa faulo aliyomufanyia Morrison na Morrison kupiga na kufunga. Hata hivyo amejitahidi sana kuonyesha kiwango kwa muda mrefu#meridianbettz

    Jibu

    Maoni:Mkude mefanya mengi simba ameonyesha kiwango chake

    Jibu

    Itakuwa poa.

    Jibu

    Namkubali sana mkude anastahili kuagwa kwa heshima msimbazi

    Jibu

    Ndio maana ake

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.