Sakata la Morrison Kucheza Mechi 2 Bila Mkataba Lafika TFF

Kamati ya Katiba, Sheria na Hadhi za wachezaji ya Shirikisho la Soka nchini (TFF) imesema kwamba hakuna mchezaji aliyeruhusiwa kucheza ligi bila ya kuwa na mkataba, hivyo kauli ya Bernard Morrison kuwa alicheza mechi mbili bila mkataba ni uongo.
Kamati ya katiba, sheria na hadhi ya wachezaji ya  TFF imesema kwamba hakuna mchezaji aliyeruhusiwa kucheza ligi kuu bila ya kuwa na mkataba.
Kauli hiyo imetolewa na mwenyekiti wa kamati hiyo, Elius Mwanjala, ametoa kauli hiyo akitolea ufafanuzi alichokisema mchezaji Bernard Morrison kuwa aliitumikia Yanga katika michezo miwili bila ya kuwa na mkataba.
Mwanjala amesema kauli ya Bernard Morrison ni ya uongo kwa kuwa utaratibu wa wachezaji wote kucheza Ligi Kuu unafahamika, ni lazima awe na mkataba ili kupata usajili na uhalali wa kucheza ligi kuu.
Kuhusu  masuala ya mkataba wa Morrison, Mwanjala amesema wanasubiri kupokea baadhi ya nyaraka kutoka Yanga ili kufahamu uhalali wa mkataba wa miaka miwili ambao mchezaji anakana kuwa hajausaini.
Hata hivyo kamati hiyo imekiri kuipokea mikataba ya miezi sita na miaka miwili ya mchezaji huyo lakini wanasubiri kikao cha mwisho kuzipitia nyaraka zitakazowasilishwa na Yanga.
Katika hatua nyingine mwenyekiti huyo amesema wanaendelea kushughulikia malalamiko ya Yanga ambao waliyafikisha  katika kamati yao juu ya moja ya klabu nchini kutumika kumrubuni mchezaji wao Bernard Morrison kiasi cha kuukana mkataba wao.
Vilevile kamati imesema itatoa hukumu ya pamoja dhidi ya Makamu Mwenyekiti wa Yanga, Fredrick Mwakalebela, ambaye amelalamikiwa kuleta taharuki ndani ya Wekundu wa Msimbazi kwa kutangaza katika vyombo vya habari kuwa wamekamilisha mazungumzo na kiungo wao Clautius Chama, kinyume na utaratibu.

45 Komentara

    Jambo hili si sawa kabisa jambo aliweza kuiyumbisha yanga kwa kipindi fulan kwa kukosa huduma yake

    Jibu

    Ni vizur San TFF kusimamia ilo

    Jibu

    Sidhani Kama ni sahihi

    Jibu

    😀😀😀watani zangu wamefulia

    Jibu

    Asante kwa taarifa#meridianbettZ

    Jibu

    Safii

    Jibu

    Ishu ya Morison ni ngumu Sana inatakiwa tamko litoke kwa viongozi nn tatizo kuhusu mchezaji Huyo na wamefikia wapi hadi sasa.

    Jibu

    Yanga wamegundua kuna kitu kinaendelea baina ya kiungo mshambuliaji wao, Bernard Morrison na baadhi ya watu wa Simba. Morrison hakuwepo kwenye kikosi cha Yanga kilichowavaa Mwadui juzi mjini Shinyanga, baada ya kuwazimia simu viongozi siku ya kuondoka Ijumaa asubuhi huku akiwaambia wenzake kwamba, bado ana hofu na virusi vya corona. Awali, nyota huyo aliyekaa kwenye mioyo ya mashabiki wa Yanga baada ya kuwafunga Simba, aligoma kusafiri kwa basi na wenzake lakini hata alipopewa tiketi ya ndege akaingia mitini. Mmoja wa vigogo wa Yanga amesema kuna habari wamezisikia kuwa kuna kigogo mmoja wa Simba alimpa mchezaji huyo kishika uchumba cha dola 10,000 (Sh23milioni). Mkataba wa miezi sita wa Morrison na Yanga unaelekea ukingoni na tayari walishasaini mkataba mwingine wa miaka miwili zaidi ambapo tayari mkataba huo upo Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) ingawa inadaiwa kwamba, haujakamilika katika baadhi ya makubaliano na hapo ndipo Mghana huyo ameanza kuwashika pabaya. Kwa upande wake Morrison, amesema kuwa ataungana na kikosi Dodoma kwa ajili ya mchezo wa Ligi Kuu Bara dhidi ya JKT Tanzania na kujitetea kwamba hakuweza kujiunga na kikosi Shinyanga kwa kuwa alikuwa bado na maumivu kwenye mguu hivyo aliona ni bora atulie kwanza maumivu yatulie.

    Jibu

    Safi sana

    Jibu

    Morrison anazingua,afungiwe mechi 10.

    Jibu

    Safi kabisa

    Jibu

    Good nwes..

    Jibu

    Asante kwa update za michezo

    Jibu

    Duh

    Jibu

    Bongo nyoso

    Jibu

    Ni habari nzuri

    Jibu

    Asante meridianbet kwa taarifa

    Jibu

    Safi tff

    Jibu

    Kwani mkataba wa Morrison una shida gani

    Jibu

    Mmmm!! Huyu nae wanamkuza kila siku kumpa bichwa#Meridianbettz

    Jibu

    Safi sana

    Jibu

    Hij saf sana

    Jibu

    Hongera #meridianbett

    Jibu

    Duh hii balaa

    Jibu

    Morisoni anahangaika km anataka kuama timu si aseme tu kuliko maneno mengi yy anadhani bila yy yanga haitoweza kufanya chochote

    Jibu

    Tff wanatia aibu kweli Yani muda wote huo Ndio wanajua hivi karibu ,wakati mwingine wawe wanajiongeza

    Jibu

    safi

    Jibu

    Safi sana

    Jibu

    Gudupdate

    Jibu

    TFF iko sawa kabisa

    Jibu

    Saf Sana

    Jibu

    Hii sio sahihi kabisa

    Jibu

    Hapa kuna kitu kinaendelea baina ya mchezaji wa yanga Morrison na majirani wekundu wa simba haiwezekani kila siku jipya linaibuka kwa ajili yake sasa wameguuka eeti yanga wanamtaka mchezaji wa simba chama ili iweje ikiwa bado mkataba wake haujaisha simba .

    Jibu

    Morrison anazingua sana yaani anataka kuwa juu ya timu yenyewe hana nidhamu

    Jibu

    Morrison anazingua mtoeni kabisa analinga achaneni nae

    Jibu

    Tff watende haki

    Jibu

    Mh! Hapa kuna kitu nyuma ya pazia

    Jibu

    mh!!hapa kuna kitu#meridianbettz

    Jibu

    Siyo poa

    Jibu

    Sizani Kama Morrison anafanya vizuri

    Jibu

    asanteni sana kwa taarifa maana Morrison alitaka kuvuruga vichwa vya mashabiki yanga

    Jibu

    Morrison hafanyi vzr

    Jibu

    Mpira wa Bongo una mambo sana

    Jibu

    Safii Sana TFF kuingilia Kati ilo sakata

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.