Alphonso Davies, Mwaga Maji Tucheze kama Kambale

Pembeni yangu hapa nimetoka kukifunga kitabu cha Juddy Donnely. Kinaizungumzia safari ya binadamu watatu wa kwanza kwenda mwezini. Haikuwa safari nyepesi. Walitumia zaidi ya miaka 20 kuiandaa. Wakatumia miaka tisa kuishawishi serikali ya Marekani kuwapatia kibali. Baada ya mapigano mengi, hatimae waliruhusiwa na waling’oa nanga July 20 1969.

Haikutegemewa kuwa watarudi hai. Ila baada ya siku nne walitua salama pale Kaskazini mwa bahari ya Pacific. Mpaka leo majina yao wale binadamu yamesimama kwenye kuta za majengo ya NASA pale Washington DC. Neil Armstrong, Edwin Aldrin na Michael Collins. Nawaweka kando hapo kisha naufungua ukurasa wa Alphonso Davies.

Wazazi wake waliikimbia Liberia baada ya vita kupamba moto mwaka 1999. Hawakuwa tayari kushika bunduki kwa ajili ya kutetea maisha yao. Hawakutaka kuendelea kupishana na maiti barabarani. Hawakutaka kuendelea kusikia sauti ya mabomu. Wakaamua kuondoka na kuishia Ghana Magharibi katika kambi ya wakimbizi. Huko ndipo walipompata Alphonso mwezi November mwaka 2000.

Baadae walipata mfadhili wa kuwatoa katika kambi ya wakimbizi, wakaondoka kwenda Canada, Alphonso akiwa na miaka 5. Huko ndipo alipoanza maisha. Kwa kuwa wazazi wake hawakuwa na hela ya kumpeleka katika academy ya soka, alilazimika kuchezea timu ya kuwalea watoto wa mtaani kila jioni alipotoka shule. Soka lake likaanzia hapo.

Hapo ndipo alipoonekana na Vancouver Whitecaps, wakamchukua na kumpeleka katika academy yao. Baadae akapanda timu ya wakubwa. Bayern wakafanikiwa kumsajili July 2018 baada ya rais wa Barcelona kugoma kumsajili kwa kigezo kwamba hatokei taifa lenye historia ya soka. Ndiyo huyu Alphonso Davies tunayemuona leo kule kushoto kwa Bayern Munich.

Safari ngumu namna gani. Kutoka kupanga foleni ya chakula katika kambi ya wakimbizi hadi kuwa mchezaji bora chipukizi wa Bundesliga. Kutoka kucheza mitaani Canada hadi kupigwa buti na Lionel Messi. Safari ambayo kimawazo isingewezekana kufanikiwa kama ile ya kwenda mwezini.


Drops and Wins!

Umeijua hii? Ni promosheni kabambe ya ushindi kwenye Casino ya mtandaoni ya Meridianbet! Unaweza kushinda hadi Euro 2,000,000 leo.

Soma Zaidi

32 Komentara

    Davis kijana mpambanaji Sana huyo anaonyesh ukomavu kwny soka na anahutendeah haki upande wake wa kushoto anastail tuzo ya mchezaj chipukiz wa UEFA Kama tuzo zitakuwepo msimu huu

    Jibu

    Anajua xana

    Jibu

    Alphonso Davis kwa kiwango ambacho amekionesha kwa sasa inaonesha kua amepitia magumu mengi na sasa alipopata nafasi niwakati wake wa kuomesha kiwango chake .

    Jibu

    Davis anajua sana kwa kiwango ambacho amekionyesha#Meridianbettz

    Jibu

    Anastahili tuzo..

    Jibu

    Histor yake ya maisha aliyo pitia ndio inamfanya hapambane sana ili kufikia ndoto zake.big up sana Davis tuna tegemea mengi makubwa kutoka kwako

    Jibu

    Davis yupo vizuri sana na kiwango chake cha kuchezea ligi kubwa

    Jibu

    Histor yake ya maisha aliyo pitia ndio inamfanya hapambane sana ili kufikia ndoto zake.big up sana Davis

    Jibu

    Mtu adi kufikia mafanikio fulani lazima atakuwa amepitia mambo mengi sana, Ni wakati wake sasa kushine

    Jibu

    Davis anajua San kwa historia yake hiyo na ukitaka kufikia ndot zako inapidi ukubali changamoto

    Jibu

    Anastahili tunzo mana mafanikio yake yanaonyesha kuwa hakuna mafanikio yanayokuja kwa urahisi ni kuoambana hata kama ikiwa katika hali ya chini bado unaweza kuwa juu good job

    Jibu

    Anastahili tunzo maanamafanikio yake yanaonyesha kuwa hakuna matanikio yanakuja kwa urahisi lazima upambane sana ndio uje kufanikiwa

    Jibu

    Davies yuko vizuri anajua sana

    Jibu

    Anastahili kupewa tuzo
    @meridianbettz

    Jibu

    Anastahili tuzo

    Jibu

    davies ana historia nzuri sana katika mpira

    Jibu

    Yupo vizuri Anastairi kwanacho kifanya

    Jibu

    Anastahili tunzo

    Jibu

    Yupo vizuri

    Jibu

    Kweli maisha km mlima kupanda na kushuka.

    Jibu

    Alphonso Davies historia yake iko vzur sana

    Jibu

    Mda wake sasa

    Jibu

    Alphonso yupo vizur

    Jibu

    Anastahili tuzo

    Jibu

    Ni historia ya kusisimua sana na Alphonso Davies alisema Baba yake alimufanya aipende Chelsea kwa maneno mengine moyo wake upo Stamford Bridge#meridianbettz

    Jibu

    Anastahil

    Jibu

    Yuko vizur

    Jibu

    Hapo ndipo alipoonekana na Vancouver Whitecaps, wakamchukua na kumpeleka katika academy yao. Baadae akapanda timu ya wakubwa. Bayern wakafanikiwa kumsajili July 2018 baada ya rais wa Barcelona kugoma kumsajili kwa kigezo kwamba hatokei taifa lenye historia ya soka. Ndiyo huyu Alphonso Davies tunayemuona leo

    Jibu

    Maisha haya yanahitaji uvumilivu sana

    Jibu

    Huu ndiyo wakati wake sasa

    Jibu

    Anaweza sana

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.