Hakuna Wakunitoa Simba - Mo

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Simba, Mohammed Dewji ‘Mo’ amesema hakuna mtu anayeweza kumuondoa kwenye timu hiyo kwa sasa.

Mo ambaye anafahamika kama mmoja kati ya mashabiki kindakindaki wa timu hiyo, amesema anaamini baada ya muda mchakato mzima wa uwekezaji utakamilika, lakini pamoja na watu kuwa wanazungumza mambo mengi, yeye hajali na hawezi kuondoka.

Akizungumza na Spoti Xtra jijini Dar es Salaam, bilionea huyo alisema kuwa anaamini asilimia kubwa ya watu wa Simba wanampenda na yeye ana nia njema na timu hiyo, hivyo hatishiki na wachache ambao wanampiga vita.

“Kuna mambo mengi sana yanaendelea, lakini jambo la msingi ni kwamba sina mpango wa kuondoka kwenye timu hii kwa sasa.

“Naamini kuwa kuna watu wana maneno yao, lakini wale wa Simba bado wananiunga mkono na wanataka niendelee kukaa hapa, nami napenda kuwaambia kuwa nipo na nitaendelea kuwepo labda hao wenye Simba yao waniondoe, lakini mimi siwezi kuondoka hata siku moja,” alisema.

Mo amesema kuhusu uwezo wa mtendaji mpya wa timu hiyo, Barbara Gonzalez na anaamini kuwa atafanya kazi nzuri kwa kuwa alipitishwa na Bodi ya Wakurugenzi ya Simba na siyo yeye kama inavyodaiwa.

“Barbara amekuwa chini ya Senzo Mazingisa (CEO aliyepita), kwa kipindi chote na amefanya kazi nzuri, mimi naamini ataendelea kufanya kazi nzuri na watu wanatakiwa kufahamu siyo mimi niliyempitisha kuwa CEO bali ni Bodi, kila mmoja alisema anafaa kwa kuwa wanamuamini,” alisema Mo.


SHINDA NA MERIDIANBET!

Tengeneza pesa kidijitali kwa kubashiri mbio za farasi hapa Meridianbet! Chagua nani ashinde, unakusanya mkwanja.

Cheza Sasa.

46 Komentara

    Sawa ila Wana msimbazi tunatak B 20 alizotuahid SIMBA

    Jibu

    Mtajijua wenyewe na simba yenu

    Jibu

    usiondoke ww ni nani….?

    Jibu

    Simba hawawezi kumtoa mo ndio baba yao na mama yao hata wafanyaje hawawezi

    Jibu

    Yeye Ni mpenzi wa simbaaaa@meridianbettz

    Jibu

    Hilo halina ubishi hakuna kweli wakukotoa Simba ila timiza makubaliano ya b20

    Jibu

    Nikweri Boss unacho kiongea wamekisikia akuna Kama wewe boss kubwa akuna atakae weza kukutoa kwenye madaraka ya krabu kubwa msimbazi akuna

    Jibu

    Kwa klabu kubwa yeyote inapopata mwekezaji lazima wakumuunga na kumpinga wawepo

    Jibu

    Mo na Simba damu damu ni kama Messi na Barcelona!!!

    Jibu

    Tatizo soka LA Tanzania linaingiliwa na siasa ndiomaana atufiki mbali hebu wanasiasa watuache kidogo na simba yetu

    Jibu

    Huenda kukawa na mengi nyuma ya Pazia lakini Mo kawatoa mbali sana Simba hawana jinsi zaidi ya kumuunga mkono na kuimarisha misingi yao tuu ili Soka la Tanzania liende Mbele

    Jibu

    safii kabisa mo

    Jibu

    Safi sana

    Jibu

    Hivyo ni kama kujisafisha tu atupatie pesa za klabu timu ifanye maendeleo kuliko kutupa hadith huu mwaka wa 3

    Jibu

    Mo kama mo hakuna wa kushindana nae

    Jibu

    Boss kasem mashabik tumelizk

    Jibu

    Achana nao boss kubwa piga kaz

    Jibu

    Safi

    Jibu

    Haya mo we endelea tu.

    Jibu

    Haipingiki iyo Mo na simba mpaka kieleweke#Meridianbettz

    Jibu

    Habari ya kufurahisha kwa wana simba.

    Jibu

    asante meridianbet kwa habar moto moto

    Jibu

    Usiondoke we nan hiyo timu si ya dewj ni ya wanasimba tufanyie hizo hisa si maneno tu

    Jibu

    hakuna kama mo#meridianbettz

    Jibu

    Aweiz tokea

    Jibu

    Kumbuka hapo mwanzo walikua watu na wameondoka mimi nasema bado haujakutana na fitina za soka la bongo utaachia siti mwenyewe

    Jibu

    Mo boss kubwa

    Jibu

    Mo Kisiki

    Jibu

    Hawezi kutolewa na mtu

    Jibu

    Simba yako fanya unavyotaka ilimradi ishiriki mashindano makubwa Africa na ikiwezekana ichukue mataji mengi ndipo watakapokujua ww nani

    Jibu

    Mo ambaye anafahamika kama mmoja kati ya mashabiki kindakindaki wa timu hiyo, amesema anaamini baada ya muda mchakato mzima wa uwekezaji utakamilika, lakini pamoja na watu kuwa wanazungumza mambo mengi, yeye hajali na hawezi kuondoka, Simba blood.

    Jibu

    Yuki sahihi

    Jibu

    Wewe nijembe endelea kuwepo timu simba izidi kusonga mbele#meridianbett

    Jibu

    Boss Kesha Sema Bado yupo yupo sana SIMBA NGUVU MOJA mpo#Meridianbettz

    Jibu

    Baba kasema

    Jibu

    Great Boss

    Jibu

    Huna lolote unaongea hivyo kwa sababu unapata faida ila kama simba ikiwa kombo je utakubali kupata hasara au ndio itakuwa maziwa yameingia maji ya mtoni

    Jibu

    Vzr

    Jibu

    Simba hawana jinsi zaidi ya kumuunga mkono na kuimarisha misingi yao tuu ili Soka la Tanzania liende Mbele

    Jibu

    Safiii mo

    Jibu

    mo anajua anachokifanya na anachokisema na ana mapenzi ya dhati sana na timu ya simba kwahiyo waache kumzushia maneno yasiyo na maana

    Jibu

    Saf sana mo

    Jibu

    Saf sanaa

    Jibu

    Sawa ila Wana msimbazi tunatak B 20 alizotuahid SIMBA

    Jibu

    You can definitely see your enthusiasm in the paintings you write. The arena hopes for even more passionate writers such as you who are not afraid to mention how they believe. At all times go after your heart.

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.