Neymar Afungiwa Mechi 2 Baada ya Kadi Nyekundu.

Neymar amepata adhabu ya kufungiwa michezo miwili kufuatia kuoneshwa kadi nyekundu katika mchezo wa Paris Saint- Germain dhidi ya Marseille na PSG kupokea kichapo cha 1-0 katika Ligue 1.

Hii ilikuwa ni mara ya pili mfululizo kwa Paris Saint-Germain kupoteza katika Ligue 1, ikiwa ndiyo kwanza ligi imeanza, mchezo uligubikwa fujo iliyopelekea wachezaji watano kuoneshwa kadi nyekundu.

Neymar mchezaji mwenye thamani kubwa, alikuwa mtu wa mwisho kuoneshwa kadi nyekundu baada ya kumsukuma kisogoni Alvaro Gonzalez.

Mbrazil huyo alilamika kufanyiwa kitendo cha kibaguzi na Alvaro ambaye alikataa kufanya tukio lolote liliashiria ubaguzi wa rangi.

Siku ya Jumatano kamati ya nidhamu ilisema Neymar amekuwa ni mchezaji wa tatu kupata adhabu ya kukosa mechi mbili.

Neymar Afungiwa Mechi 2 Baada ya Kadi Nyekundu.

Layvin Kurzawa yeye amefungiwa michezo sita na Leandro Paredes ambaye ni usajili mpya wa Paris Saint-Germain atakuwa nje kwa wiki mbili.

Watatu hao walishuhudia timu yao ya PSG ikipata ushindi wa kwanza tangu kuanza kwa msimu mpya wa Ligue 1 dhidi ya Metz katika mchezo huo Abdou Diallo alioneshwa kadi nyekundu.

Angel Di Maria alikuwa mkombozi wa PSG katika mchezo huo kwa kuipatia timu yake goli katika dakika za majeruhi lakini alikumbana na kamati ya maadili akihusishwa katika fujo zilizotokea kwenye mchezo dhidi ya Marseille.

Mchezaji Marseille Jordan Amavi amepata adhabu ya kuikosa michezo mitatu na Dario Benedetto ataukosa mchezo mmoja.


SHINDA NA MERIDIANBET!
Tengeneza pesa kidijitali kwa kubashiri mbio za farasi hapa Meridianbet! Chagua nani ashinde, unakusanya mkwanja.
Cheza Sasa.

44 Komentara

    Pole sana Neymar ndio mpira huo

    Jibu

    duh sio poa

    Jibu

    Duu sio poa Neymar atumikia azabu ya kukaa njee PSG wangalie mwenendo wanao endanao mwisho wake watakuja kulaumiana zaidi namwenendo wao ukawa mpaya kwenye matokeo

    Jibu

    Duuh majanga hayo Neymar ila ndio mpira ulivyo#Meridianbettz

    Jibu

    Mbona majanga

    Jibu

    Wasiangalie upande mmoja.lkn ata uyo nae aliemfanyia mwenzie matendo ya kibaguzi achukuliwe hatua

    Jibu

    Mbna maajabu tena

    Jibu

    Pole yake

    Jibu

    Mbona balaa hilo

    Jibu

    Duh sio poa

    Jibu

    Dhaa hii adhabu itaigarimu klabu yake maana watu waliogewa adhabu ni tegemezi katika klabu

    Jibu

    Sio habari nzuri

    Jibu

    Siku nyingine atajifunza kutokana na makosa

    Jibu

    Pigo kwa PSG lakini pia chama cha soka cha Ufaransa kina kazi ya kuchunguza madai ya Neymar

    Jibu

    Clabu ya PSG inawakati mgumu ukiangalia wachezaji tegemezi wote wapo nje

    Jibu

    Habari mbaya pole yake@meridianbettz

    Jibu

    Sheria inabid iangalie kwa upande wa pili maana sio adhabu nzur kwel Neymar alitolewa maneno ya ubaguz ndo maana alipatwa na hasira VAR lzma waangalie na hilo

    Jibu

    Habari njema

    Jibu

    Badnews

    Jibu

    hatar

    Jibu

    Duuh

    Jibu

    Pole ney

    Jibu

    Duuh

    Jibu

    Sio poa

    Jibu

    Jamani Neymar pole sana#meridianbettz

    Jibu

    Itaikost team kipnd ichi

    Jibu

    Duuuh majanga

    Jibu

    Daah wamemuonea alipataghazabu kwaajili ya ubaguzi alio fanyiwa daaah pole Neymar

    Jibu

    Hili nipengo kubwa Sana kwa PSG.

    Jibu

    Pole yake

    Jibu

    Pigo kwa PSG lakini pia chama cha soka cha Ufaransa kina kazi ya kuchunguza madai ya Neymar

    Jibu

    Pigo kwa psg Matajir wa paris vle vle sheria imefuata mkondo wake

    Jibu

    Pole neymar mambo yakawaida tuu kwenye michezo pale unapokosea lazima wakukumbushe wajibu wako.

    Jibu

    ilo ni funzo kwa wengine ili wawe na adabu wanapokuwa uwanjani

    Jibu

    Nidhamu muhimu popote pale

    Jibu

    Siyo poa

    Jibu

    Ubaguzi hauwezi kuisha kwenye nchi za kigeni kabisa huko barani ulaya maana tabia ukiwa tangia wapo wa dogo kudharau ngozi nyeusi

    Jibu

    Duuh pengo kubwa kwa PSG kukosekan kwa neymer kwa mech mbili.

    Jibu

    Duu pole yake

    Jibu

    Dah! Pole yake

    Jibu

    Hawajafany sahih

    Jibu

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.