Real Madrid wameripotiwa kuwa wanamuaona mshambuliaji wa Inter Milan Romelu Lukaku kama mbadala wa muda mrefu wa Karim Benzema.
Lukaku amekuwa katika fomu nzuri kwa klabu yake ya Italia tangu kuanza kwa kampeni ya msimu huu 2020-21, akipata magoli mara tisa katika mechi tisa za mashindano yote.
Wakati huo huo, mchezaji huyo wa kimataifa wa Ubelgiji amefunga jumla ya mabao 43 katika mechi 60 tu akiwa na kikosi cha Antonio Conte tangu alipowasili kutoka Manchester United msimu wa joto wa 2019.

Benzema bado ni mchezaji muhimu kwa kikosi cha Zinedine Zidane, lakini Mfaransa huyo atakuwa na umri wa miaka 33 mwezi ujao, na Los Blancos wanafikiria kuangalia mbadala wa mshambuliaji huyu wa muda mrefu.
Kulingana na ripoti huko Uhispania, rais wa Madrid Florentino Perez anamwona Lukaku, ambaye ana kandarasi San Siro hadi mwisho wa kampeni ya msimu wa 2023-24, kama mbadala anayeweza kusainiwa.
Mchezaji huyo wa miaka 27 anadaiwa alikuwa kwenye rada za uhamisho za Manchester City msimu wa joto. Huenda safari yake ikaendelea upande wa La Liga.
Hadi 130,000,000 TSH Kutolewa kwa washiriki wa shindano la Playson Cashfall. Unaipata kwenye Kasino ya Mtandaoni ya Meridianbet Pekee. Jisajili sasa, kisha ingia mchezoni kabla ya Novemba 29.



Dorophina
Big deal kwa lukaku
magdalena
lukaku kapata bonge nono la deal kila la kheri
Samira
Lukaku naona anazidi kung’aa tu
Adelta
Lukaku anazidi kuwa kinara
Nasra
Lukaku mtu mbaya
Tatu
Lukaku anazidi kuwa kinara
Ester jackson
Inter Milan wamepta mchezaji mana hasaivi namuona yuko vizuri zaid
Khadija
Lukaku anazid kuwa juu
Lydia Emmanuel Magoti
Lukaku anataka kulamba dume hapo
Saupha mohamed
Lukaku yupo vuzuri
Sarah
Lukaku yupo vizuri
aisha
Lukaku namkubali sana
Genia Sikaluzwe
Lukaku naona anazidi kung’aa tu
Hopemwaikuka
Am happy for luka
Fatina mfingi
Lukaku yuko vizur san namkubal
Sauda
Dili nono kwa Lukaku
warda
romelu ataweza kweli