Baada ya kufanya vizuri na kujitengenezea jina kubwa kwenye ulimwengu wa ndondi, bondia Anthony Joshua amejitolea kuwasaidia mabondia wachanga nchini Uingereza.
Anthony Joshua ameamua kuwashika mikono mabondia wanaochipukia akiamini kuwa anajukumu la kuwaendeleza watoto na vijana wa kizazi kijacho.
Kwa kuamini hilo, AJ ametoa mtonyo mrefu na kuahidi kujitolea kufanya mazoezi na mabondia wachanga kama sehemu ya kuwapatia motisha na kuamini chochote kinawezekana.
Akizungumza na Dan Roan wa BBC Sport, AJ amesema “bila ya kuwa na mashindano ya chini, hakuna Anthony Joshua. Milango ya sehemu hizi za mazoezi ipo wazi kwa mabondia wote wachanga kutoka kwenye mazingira yeyote.

“Kama ningeweza kurudi kwenye miaka 18 na sehemu zote za mazoezi ziwe zimefungwa kama hivi, ningevunjika moyo sana.
“Sio msaada wa fedha tu. Nitajitahidi kuwapa motisha hawa watoto kwa kuwa sehemu yao, nitashusha mikanda yangu na kufanya nao mazoezi.
“Ninaamini katika miaka 10-15 ijayo, tutawaona viongozi wa kesho, lakini siamini kama ni miaka 25-30 kwasababu tumeshakipoteza hiki kizazi.”

AJ aliianza safari yake ya kuwa bondia mkubwa duniani baada ya kushinda medali ya dhahabu kwenye mashindano ya Olympic 2012 wakati ule akiwa kama bondia mchanga.
2016 AJ alikuwa bingwa wa dunia baada ya kumburuza Mmarekani – Charles Martin ambapo aliibuka na mkanda wa IBF.
VUNA SHEA YAKO YA 230,000,000TSH NA UFURAHIE MSIMU HUU WA SIKUKUU!!!
Kupitia Kasino ya Mtandaoni ya Meridianbet, jiwekee nafasi ya kupata shea yako ya 230,000,000Tsh kupitia mchezo wa Secret Santa. Hakika hutojutia kufurahia msimu huu wa sikukuu ukiwa katika nyumba ya mabingwa ya Meridiabet. Unasubiri nini???



Adelta
Ni miongoni mwa mabondiya wanaopenda kuona mafanikio ya wenzao
Caroline
Ni jambo zuri
Angelina
Safi ni uamuzi mzuri
Sarah
Safi sana niuwamuzi mzuri
Magdalena
Jambo jema
Rahmal
Jambo zuli
Issa
Joshua anajitoa sana
Hopemwaikuka
God bless you
Saupha mohamed
Jambo zuri
Tatu
Jambo zuri
Mwanahamisi
Jambo jema
Lydia Emmanuel Magoti
Safiii Sana kafanya Wema zaidi kwa ware wanao taka kuinuka zaidi
warda
Ndo vizuri
Ernest Kimeru
Jambo zuri