Baada ya miaka mitano kupita tangu aondoke hatimaye Dani Alves amerejea katika klabu ya Barcelona kwa mara nyingine kwa uhamisho huru.

Beki huyo wa kulia (38) ataanza mazoezi na timu wiki ijayo lakini hataweza kucheza na kikosi cha The Blaugrana mpaka Januari na amesaini dili mpaka mwisho wa msimu.
Dani Alves ni moja ya beki namba mbili bora katika historia ya Barca na wameshindwa kupata mbadala wake tangu kuondoka kwake, baada ya kuhamia PSG na Sao Paulo sasa amerudi kwenye nafasi yake huko Camp Nou.
“Takriban miaka mitano ya kupigana kama kichaa kufikia hatua bora. Sikujua ingedumu kwa muda mrefu, sikujua ingekuwa ngumu sana,” Alves aliandika kwenye Instagram.
“Lakini nilijua ndani ya moyo wangu na ndani ya roho yangu kuwa siku hii itafika. Ninarudi nyumbani mahali ambapo sikuwahi kuondoka.
“Tutaonana hivi karibuni tukiwa na nia sawa ya kusaidia kujenga upya klabu bora zaidi duniani
Unawezaje kuikosa hii! njia rahisi ya kutengeneza mkwanja katika kasino maridhawa za meridianbet. Muda wa kufurahia na kutengeneza mkwanja ipo mikononi mwako unasubiri nini?


