Kocha wa klabu ya Real Madrid Carlo Ancelotti wakati akijiandaa na mchezo wa nusu fainali ya ligi ya mabingwa ulaya dhidi Man City aliulizwa kuhusu mbio za ubingwa nchini italia alisema kuwa ni aina ya ushindani ambao hatujauona kwa muda mrefu.
Kwenye mashindano ya ligi ya mabingwa ulaya ni yeye pekee kocha mkongwe aliyebakia kwenye hatua ya nusu fainali ambapo mchezo wake wa kwanza dhidi ya Man City utapigwa kwenye dimba la Etihad.
![]()
Ancelotti amaetumia muda wake mwingi kwenye soka la Italia ambako na ko alifanikiwa kuifundisha klabu ya Ac Milan na muda mwingi huwa anafuatilia muenemdo wa ligi hiyo ya Serie A.
Wakati akihojiwa na Sky Sport Italia kuhusu mbio za ubingwa wa Serie A na kufuatilia kwa ligi hiyo alijibu, “bila shaka nafuatilia mpira wa Italia, Rossoneri walipata ushindi muhimu usiku wa jana dhidi ya Lazio, inakwenda kuwa mpambano mzuri wa nafasi ya ubingwa,ni aina ya ushindani ambao hatujauona kwa kipindi kirefu nchini Italia.
“Kiuhalisia, naamini Milan atashinda”
Una Kila sababu ya kufurahia wiki yako na kutengeneza mwaka huu uwe wa faida zaidi katika kasino zetu za mtandaoni za meridianbettz. Mchezo wa Zeus Ancient Fortunes unakuongoza kutekeleza hilo.


